• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

imewekwa Tar: July 21st, 2025

Khadija Dalasia - Nkasi ,Rukwa 

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere, leo Julai 21,2025 ameongoza kikao kazi na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi na kutoa pongezi kwa usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo, hususan kwenye sekta za Afya, Elimu na Maji. 

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri, Mheshimiwa Makongoro aliwapongeza watumishi hao kwa kuonesha mshikamano, uwajibikaji na moyo wa kizalendo katika utekelezaji wa majukumu yao, hali iliyowezesha miradi ya maendeleo kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa. “Ninawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayoifanya. Miradi yetu ya Afya, Elimu na Maji inatekelezwa vizuri na inakamilika kwa wakati. Huu ni ushahidi tosha wa usimamizi bora na umoja miongoni mwenu,” alisema Mheshimiwa Makongoro. 

Aidha, Mkuu wa Mkoa amewataka kuendeleza moyo wa kujituma, kushirikiana kwa karibu na kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja na miradi hiyo kwa kupata huduma bora, zenye tija na zinazogusa maisha yao ya kila siku. Kikao hicho ni sehemu ya ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuzungumza na watumishi wa umma katika halmashauri zote za mkoa wa Rukwa. 

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa amekagua miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule ya Msingi Chima, ujenzi wa madarasa na mabweni katika shule ya Sekondari Chala, ujenzi wa shule ya amali ya wilaya Londokazi, ujenzi wa shule ya amali ya Mkoa iliyopo kata ya Majengo,ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Kata ya Isunta, ukamilishaji wa nyumba za watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Nkasi.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA - 2025, KULINGANA NA MATOKEO YALIYOTANGAZWA NA BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA (NECTA) June 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RUKWA YAENDELEA KUCHUKUA HATUA THABITI KUDHIBITI VIFO VYA MAMA NA MTOTO

    July 28, 2025
  • RUKWA YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU JUMUISHI YA TAIFA YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO

    July 24, 2025
  • INEC YAWATAKA WATENDAJI WA UCHAGUZI KUZINGATIA VIAPO VYAO NA MAADILI YA KAZI

    July 23, 2025
  • INEC YAWATAKA WATENDAJI WA UCHAGUZI KUZINGATIA VIAPO VYAO NA MAADILI YA KAZI

    July 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa