• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

imewekwa Tar: September 30th, 2025



Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 zimeendelea leo Septemba 30,2025 katika Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, huku miradi mbalimbali ya maendeleo ikiendelea kuzinduliwa,kukaguliwa na kuwekewa mawe ya msingi.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025, Ndg. Ismail Ali Ussi, amesema kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta za elimu na maendeleo ya jamii zinatafutiwa ufumbuzi wa kudumu.


Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika Shule ya Sekondari Mbuluma, wilayani Kalambo, Ndg Ismail Ali Ussi amesisitiza kuwa uwekezaji katika elimu ni msingi wa maendeleo endelevu ya taifa. Amesema ujenzi wa shule hiyo ni hatua muhimu ya kuwawezesha watoto wa kike na wa kiume kupata elimu katika mazingira rafiki na salama.


Wananchi wa kijiji cha Mbuluma wameeleza kufurahishwa kwao na ujenzi wa shule hiyo, wakisema kuwa itapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto za mimba na ndoa za utotoni. Wamesema awali wanafunzi walilazimika kutembea zaidi ya kilomita 20 kwenda shule ya kata jirani, hali iliyosababisha wengi wao kukata tamaa ya kuendelea na masomo.


Mbali na sekta ya elimu, kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge ameweka jiwe la msingi katika daraja la Mto Mao. Kabla ya kuanza kwa ujenzi wa daraja hilo hali ya maisha ya wananchi ilikuwa hatarini hasa nyakati za mvua, kutokana na kukosa miundombinu imara ya kuvukia. Wananchi wa eneo hilo wamesema kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutapunguza ajali na vifo, na pia kufungua fursa za kibiashara kwa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa ndani na nje ya wilaya hiyo.


Jumla ya miradi nane yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.9 imezinduliwa, kukaguliwa na kuwekewa mawe ya msingi katika Wilaya ya Kalambo kupitia Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka huu. Miradi hiyo inajumuisha sekta za elimu, miundombinu na maendeleo ya jamii.


Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo cha kuhamasisha mshikamano wa kitaifa, uzalendo na uwajibikaji, huku ukimulika kwa ukaribu utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa