• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mhandisi Nyamuhanga apongeza kituo cha afya Mazwi Sumbawanga.

imewekwa Tar: December 18th, 2019

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamuhanga amepongeza juhudi zinazofanywa na watumishi kituo cha afya cha Mazwi, Manispaa ya Sumbawanga baada ya kuona namna wanavyokabiliana na ongezeko la wateja wanaohitaji huduma za afya katika kituo hicho ambacho huzalisha wajawazito wapatao 373 kwa mwezi.

Amesema kuwa kabla ya hapo kituo hicho kilikuwa kidogo sana na kushindwa hata kutoa huduma za upasuaji jambo ambalo lilipelekea hospitali ya rufaa ya mkoa kuzidiwa na wagonjwa lakini hali hiyo kwa sasa ni tofauti baada ya upanuzi wa kituo hicho ambacho kutokana na huduma zake wateja wengi huvutiwa kufika na kupata huduma.

Amesema kuwa serikali inatoa fedha nyingi kupata dawa pamoja na vifaa tiba hivyo kinachotegemewa katika kituo hicho ni huduma bora ya afya na kuongeza kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli imejenga vituo vya afya zaidi ya 352 ambapo mojawapo ya vituo hivyo ni kituo cha afya cha Mazwi katika Makispaa ya Sumbawanga ambapo walipatiwa shilingi milioni 500 na sasa kituo hicho kimekamilika na kuanza kutoa huduma.

“Nimefurahishwa kwa upanuzi ambao umefanyika katika kituo hiki cha Mazwi, kilikuwa kituo kidogo tu nakumbuka siku za nyuma lakini kimekarabatiwa kimekuwa kituo kizuri na kinapendeza lakini kitu cha kufurahisha ni kwamba kinahudumia wateja wengi lakini na huduma inayotolewa hapa nimetoka kukagua katika maeneo mbalimbali katika wodi kwakweli nimeridhika na huduma ambazo zinatolewa, changamoto ni kwamba wameongezeka wateja baada ya ukarabati kufanyika, tunashukuru wataalamu wetu wanajitahidi kuwahudumia,” Alisema.

Wakati akitoa taarifa ya kituo cha Afya cha Mazwi Mganga Mkuu wa halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga Dkt. Archie Hellar alisema kuwa kuanzia mwezi Januari hadi Novemba kituo hicho cha afya kimezalisha wajawazito 4,103 na kati ya hao waliofanyiwa upasuaji ni wajawazito 426 na kupatikana vifo viwili kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo katika harakati za kuwafanyia wajawazito hao upasuaji..

“Kwajhiyo changamoto tunazozipata ni kwamba wateja ni wengi zaidi wanaichukulia hospitali hii ni kama ya mkoa na wengine wanatoka nje ya manispaa n ahata nje ya Wilaya nyingine kuja kujifungua hapa, sasa ukilinganisha watumishi pamoja na rasilimali fedha unakuta kituo kinaelemewa, lakini hata hivyo tunajitahidi kwa kushirikiana na Mkurugenzi wetu wa manispaa Jacob Mtalitinya kwakweli anatiupa nguvu na kutusaidia sana kufanikisha kutoa huduma,” Alisema.

Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ilipata shilingi milioni 500 za kupanua ujenzi wa kituo cha Afya cha Mazwi pamoja na kupewa shilingi milioni 400 kwaajili ya ujenzi wa kituo cha Afya kipya kilichopo katika kata ya Katumba azimio ikiwa ni kilometa 12 kutoka katika kituo cha afya cha Mazwi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa