• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MHESHIMIWA MAKONGORO AKAGUA MIRADI WILAYANI NKASI, ATAKA KASI ZAIDI YA UTEKELEZAJI

imewekwa Tar: November 19th, 2025

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere, amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo Wilayani Nkasi leo Novemba 19, 2025, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kufuatilia utekelezaji wa miradi na matumizi sahihi ya fedha za umma. 

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Makongoro amekagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa katika sekta za afya, elimu, maji na utawala, huku akiwataka wasimamizi kuhakikisha kazi zote zinafanyika kwa viwango vinavyokubalika na kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali. Amesisitiza kuwa nidhamu ya matumizi ya fedha, ufuatiliaji wa karibu na kasi ya utekelezaji ni msingi muhimu wa kufanikisha malengo ya Serikali. 

Katika sekta ya elimu, Mkuu wa Mkoa ametembelea Shule ya Sekondari Milundikwa ambako ujenzi wa madarasa na majengo ya msingi unaendelea. Aidha, ametembelea ujenzi wa miundombinu ya kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Chala pamoja na ujenzi wa Shule ya Amali ya Mkoa. Amesema ni muhimu kuhakikisha ubora wa kazi, upatikanaji wa vifaa kwa wakati, na kukamilika kwa miradi ndani ya muda uliopangwa ili wanafunzi wapate mazingira bora ya kujifunza. 

Ametoa maagizo ya kuongeza kasi katika maeneo yote ambayo utekelezaji bado unasuasua. Akizungumza na watendaji na wananchi waliokusanyika katika maeneo mbalimbali ya ukaguzi, Mheshimiwa Makongoro amepongeza ushirikiano unaooneshwa katika kusukuma mbele miradi ya maendeleo. Amehimiza jamii kuendelea kulinda miundombinu inayojengwa na kuitumia kwa manufaa ya wote. 

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake kwa kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Chala na kutembelea mradi wa maji wa Namanyere pamoja na ukarabati wa ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi. Ziara hiyo imelenga kuimarisha uwajibikaji, kuongeza ufanisi wa usimamizi wa miradi na kuhakikisha kila fedha ya Serikali inaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa