• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MHESHIMIWA MAKONGORO ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU 2025; AWAALIKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI

imewekwa Tar: September 26th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere, amesema kuwa maandalizi ya kupokea Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 katika Mkoa wa Rukwa yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha, na amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi hayo kama ishara ya mshikamano na kuunga mkono juhudi za maendeleo.


Akizungumza na vyombo vya habari leo Septemba 26, 2025 ofisini kwake, Mheshimiwa Makongoro ameeleza kuwa Mkoa wa Rukwa unatarajia kuupokea Mwenge wa Uhuru siku ya Jumapili, tarehe 28 Septemba 2025, katika Kijiji cha Kizi, Kata ya Paramawe, Tarafa ya Namanyere, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi.


Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa kuanzia tarehe 28 Septemba hadi 1 Oktoba 2025, ambapo utakimbizwa umbali wa kilomita 653.1. Katika kipindi hicho, Mwenge wa Uhuru utakagua, utaweka mawe ya msingi, na kuzindua jumla ya miradi 34 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 55.3.


Mheshimiwa Makongoro pia ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi wote waliojiandikisha na wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu. Amesisitiza kuwa kupiga kura ni haki ya kikatiba ya kila mtanzania, na ni njia halali ya kushiriki katika kuamua mustakabali wa taifa.


Aidha, ameeleza kuwa ushiriki wa wananchi katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru si tu ni ishara ya uzalendo, bali pia ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Rukwa.


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amewahimiza viongozi wa Serikali, taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha kuwa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2025 yanakuwa ya mafanikio makubwa na yenye kuhamasisha mshikamano wa kitaifa.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MANISPAA YA SUMBAWANGA, MIRADI YA BILIONI 30.3

    September 29, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI WILAYANI NKASI; KIONGOZI ATAKA WANANCHI WATUMIE FURSA YA ELIMU YA UFUNDI

    September 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOANI RUKWA; KUKIMBIZWA KWA SIKU NNE; KUMULIKA MIRADI YA BILIONI 55.3

    September 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa