• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MHESHIMIWA MAKONGORO ATOA WITO WA USHIRIKIANO KATIKA KUIMARISHA ELIMU YA LISHE

imewekwa Tar: September 18th, 2025

MHESHIMIWA MAKONGORO ATOA WITO WA USHIRIKIANO KATIKA KUIMARISHA ELIMU YA LISHE


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere, ametoa wito kwa viongozi wa Serikali, taasisi za dini, jamii na vyombo vya habari kushirikiana kikamilifu katika kutoa elimu ya lishe bora kwa wananchi, ili kusaidia kuimarisha afya na maendeleo ya watoto na vijana.


Akizungumza leo Septemba 18, 2025 katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa (RDC), Mheshimiwa Makongoro ameeleza kuwa lishe duni bado ni changamoto kubwa inayoathiri ukuaji wa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, hali inayochangia udumavu na matatizo ya kiafya kwa watoto katika Mkoa wa Rukwa na taifa kwa ujumla.


"Ni wajibu wa kila kiongozi kutumia kila jukwaa analopata kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa lishe bora. Nawaomba viongozi wa dini wasaidie kufikisha ujumbe huu katika nyumba za ibada, wataalamu waendelee kutoa miongozo sahihi ya lishe, na vyombo vya habari viendelee kuelimisha jamii kupitia vipindi na makala,"amesema Mheshimiwa Makongoro.


Licha ya Mkoa wa Rukwa kupata wastani wa asilimia 85 katika tathmini ya kitaifa ya utekelezaji wa afua za lishe, Mheshimiwa Makongoro amebainisha kuwa bado kuna changamoto ya kutotengwa kwa rasilimali fedha za kutosha katika Halmashauri za Mkoa wa Rukwa kwa ajili ya kutekeleza afua hizo muhimu kama ilivyokubaliwa kwenye Mkataba wa Lishe.


Aidha,amewataka wajumbe wa kikao hicho kuhakikisha kuwa mipango na bajeti za lishe zinawekewa vipaumbele katika Mwaka wa Fedha unaofuata, huku akisisitiza kuwa taifa lenye viwango vya juu vya udumavu haliwezi kufikia maendeleo endelevu.


“Tusimame pamoja kama Mkoa kuhakikisha kuwa tunawekeza ipasavyo katika lishe, kwa sababu taifa lenye watoto na vijana wenye udumavu ni taifa lenye changamoto katika nguvu kazi, elimu na uchumi. Ushirikiano wetu ndio msingi wa mabadiliko ya kweli,”amesisitiza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa.


Kikao hicho kimehudhuriwa na wakuu wa idara, wawakilishi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Rukwa, wawakilishi wa taasisi zisizo za kiserikali,viongozi wa dini na wadau mbalimbali wa sekta ya lishe.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa