• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MHESHIMIWA MAKONGORO AZINDUA KITUO CHA POLISI CHALA, AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA MAENEO YA UJENZI WA VITUO VYA POLISI

imewekwa Tar: September 20th, 2025


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere, ameziagiza Halmashauri zote ndani ya Mkoa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Polisi katika kila Kata, ikiwa ni mkakati wa kuimarisha usalama wa wananchi na mali zao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa jengo la Kituo cha Polisi cha Kata ya Chala, wilayani Nkasi, uliofanyika Septemba 20, 2025, Mheshimiwa Makongoro ameeleza kuwa usalama wa wananchi ni kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Katika hotuba yake, Mheshimiwa Makongoro ametaka kila Halmashauri kuhakikisha inatenga ardhi yenye hati miliki kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Polisi, akisisitiza kuwa maeneo hayo hayapaswi kubadilishiwa matumizi bila idhini ya Serikali.


Aidha, amewaasa wananchi wa Kata ya Chala kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuimarisha usalama, akisisitiza kuwa jeshi hilo si adui wa wananchi bali ni chombo muhimu cha ulinzi wa raia na mali zao.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Shadrack Masija, ametoa onyo kali kwa watu wote watakaojihusisha na vitendo vya hujuma dhidi ya miundombinu ya Jeshi la Polisi, akibainisha kuwa Serikali inatumia rasilimali nyingi za walipa kodi katika ujenzi na uboreshaji wa vituo hivyo.


Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Chala umegharimu shilingi milioni 115, na unatarajiwa kutoa huduma kwa zaidi ya wananchi 68,000 wa Kata ya Chala pamoja na vijiji na maeneo jirani.


Wananchi waliohudhuria hafla hiyo wameipongeza Serikali kwa hatua hiyo, wakieleza kuwa kituo hicho kitasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matukio ya uhalifu yaliyokuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika maeneo ya pembezoni mwa Kata hiyo.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MANISPAA YA SUMBAWANGA, MIRADI YA BILIONI 30.3

    September 29, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI WILAYANI NKASI; KIONGOZI ATAKA WANANCHI WATUMIE FURSA YA ELIMU YA UFUNDI

    September 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOANI RUKWA; KUKIMBIZWA KWA SIKU NNE; KUMULIKA MIRADI YA BILIONI 55.3

    September 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa