• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Miaka 60 ya Uhuru

imewekwa Tar: December 8th, 2021

RC MKIRIKITI: MIAKA 60 YA UHURU IFANYE WATUMISHI WA UMMA KUSHIKAMANA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amewataka watumishi wa umma kutumia sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara kuendeleza amani na mshikamano mahala pa kazi.

Ametoa wito huo leo (08.12.2021) wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru ambapo amewapongeza kwa kazi nzuri iliyochangia maendeleo ya taifa.

" Nimekuja hapa kuwapongeza watumishi wote wa Manispaa kwa niaba ya watumishi wengine wa umma wa mkoa wa Rukwa kwa kazi nzuri mliyofanya hata leo Taifa letu linafikia mafanikio ya miaka 60 ya kuwa huru. Endeleeni kuwa wazalendo kwa taifa letu " alisema Mkirikiti.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Jacob Mtalitinya watumishi wametakiwa kuendelea kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia haki,upendo na mshikamano .

Mkirikiti alitumia fursa hiyo kuwataka watumishi hao kuongeza jitihada ili manispaa ya Sumbawanga iwe na maendeleo ikiwemo mapato ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alikemea pia tabia ya ubinafsi miongoni wa viongozi ndani ya manispaa hiyo hatua inayopelekea kuwepo malalamiko mengi ya watumishi kutopata haki zao na mlundikano wa madeni .

" Nataka Idara ya Utumishi ilipe madeni ya watumishi. Tafuteni fedha kwa kukusanya mapato kwa vyanzo vyenu vyote ili watumishi na wazabuni wanaodai walipwe kwa haraka. Halmashauri yenu sasa haina afya kiuchumi. Badilikeni " alisema Mkirikiti.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka watumishi wote wa serikali mkoani humo kuanza siku ya kwanza baada ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara hapo kesho kwa kubadilika kiutendaji ili wananchi waweze kunifaika kwa kupata huduma bora zinazotakiwa kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryuba alisema Mkurugenzi wa halmashauri hiyo anapaswa kubadilika na kuwa karibu na watumishi kwa kutanguliza utatuzi wa kero zao ili shughuli za kuleta maendeleo zisikwame.

" Mkurugenzi umesikia aliyosema Mkuu wa Mkoa, weka muunganiko kati ya watumishi na wakuu wa idara wako . Umoja na mshikamano ukiwepo tutaongeza kasi ya manispaa kustawi " alisema Waryuba.

Mkoa wa Rukwa leo unaadhimisha Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara Kimkoa  katika sherehe zitakazofanyika kijiji cha Kaengesa wilaya ya Sumbawanga.

Mwisho.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa