• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MIAKA MITATU YA AWAMU YA SITA; UWEZESHAJI SEKTA YA ELIMU RUKWA WAPAA

imewekwa Tar: April 2nd, 2024


Na _Khadija Dalasia-Rukwa_

Katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya awamu ya Sita, Mkoa wa Rukwa umeshuhudia maendeleo makubwa katika Sekta ya Elimu. Kiasi cha shilingi bilioni 64.7 zimetumika kujenga na kuimarisha miundombinu ya elimu ya Msingi, Sekondari, Vyuo vya Kati na Elimu ya Juu.

Jumla ya shule mpya 36 za Msingi na Sekondari zimejengwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Halmashauri za Wilaya za Kalambo, Nkasi, na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga.

Mkoa wa Rukwa umepokea kiasi cha shilingi bilioni 15.3 kwa ajili ya elimu ya Msingi na shilingi bilioni 26.1 kwa ajili ya elimu ya Sekondari katika kipindi hicho. Ujenzi na maboresho ya miundombinu ya elimu kwa ujumla umepunguza changamoto ya umbali na msongamano wa wanafunzi kwa miundombinu michache iliyokuwepo. Pamoja na hayo Serikali imeboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu.

Aidha, upanuzi wa taasisi za elimu katika ngazi zote, kama vile ujenzi wa miundombinu mipya katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya Tawi la  Rukwa, ujenzi wa miundombinu mipya ya Chuo cha Ualimu Sumbawanga na ujenzi wa Chuo cha Veta Mkoani Rukwa unaendelea kuthibitisha dhamira ya Serikali ya kutanua wigo wa utoaji wa elimu kwa wananchi wake. Jumla ya shilingi bilioni 23 zimewekezwa na Serikali kwa maboresho hayo.

Matokeo ya uwekezaji mkubwa katika Sekta ya Elimu Mkoani Rukwa yameanza kuonekana. Idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika ngazi mbalimbali imeongezeka. 

Katika kipindi cha miaka mitatu ya uwekezaji huo idadi ya wanafunzi walioandikishwa kujiunga na elimu ya msingi imeongezeka kutoka 46,526 kwa Mwaka 2021 hadi 63,666 kwa Mwaka 2024 sawa na ongezeko la asilimia 36 huku idadi ya wanafunzi waliojiunga na elimu ya Sekondari ikiongezeka kwa asilimia 9 kutoka wanafunzi 315,887 Mwaka 2021 hadi kufikia 346,787 kwa Mwaka 2024.

Ongezeko hilo ni matokeo ya mpango wa elimu bila malipo na maboresho makubwa ya  miundombinu.

Kwa ujumla, Mkoa wa Rukwa umeshuhudia mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu katika kipindi cha Mwaka 2021 mpaka 2024. Mabadiliko hayo yanaithibitisha nia ya Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuweka mazingira bora ya kujifunza na kujifunzia ili kuinua kiwango cha elimu na ujuzi kwa wananchi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa