• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mikataba Lishe

imewekwa Tar: October 19th, 2022

USTAWI WA FAMILIA UNATEGEMEA LISHE BORA- RC SENDIGA

Na. OMM Rukwa

Halmashauri za mkoa wa Rukwa zimesema zitaendelea kuhakikisha zinatenga na kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji afua za lishe ili kukabiliana na tatizo la udumavu na utapiamlo kuathiri afya ya watoto chini ya miaka mitano

Akizungumza kwa niaba ya madiwani wa mkoa wa Rukwa, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justin Malisawa alisema wakiwa wasimamizi wakuu wa halmashauri watahakikisha kila robo mwaka fedha za afua za lishe zinatengwa na kutolewa kwa jamii.

Malisawa amesema hayo leo (Oktoba 19, 2022) mjini Sumbawanga wakati wa hafla ya utiaji saini mikataba ya utekelezaji afua za lishe kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga na Wakuu wa Wilaya za Sumbawanga, Nkasi na Kalambo.

“Sisi madiwani tutaendelea kuhakikisha kila matumizi ya halmashauri ya miezi mitatu fedha za lishe zinatengwa na kupelekwa katika utekelezaji wa agenda za lishe .Suala la lishe endelevu litaendelea kupewa kipaumbele”alisema Malisawa.

Akifungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga aliwataka wakuu wa wilaya kuhakikisha mikataba waliyosaini inakwenda kutekelezwa hadi ngazi ya chini kwa watendaji kabla ya ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.

Sendiga alibainisha kuwa mkataba huo ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kunakuwa na utekelezaji wa afua mbalimbali za lishe katika jamii ili kupunguza kiwango cha udumavu ambacho mkoa wa Rukwa ni asilimia 47.9.

“Maelekezo yangu kwa Wakuu wa Wilaya, mkasimamie wilaya zenu kuhakikisha fedha zilizopangwa kutekeleza afua za lishe zinatolewa kwa wakati. Aidha, taasisi zote zinazoshughulikia suala la lishe katika mkoa zijulikane ili iwe rahisi kufuatilia mipango yao utekelezaji “alisisitiza Sendiga.

Naye Mratibu wa Mradi wa Lishe Endelevu mkoa wa Rukwa Maria Machilu alisema suala la vikao vya kamati za lishe lipewe kipaumbele kwenye halmashauri ili kuwezesha jamii kushiriki kupanga mikakati ya kupunguza udumavu ikiwemo elimu ya lishe bora.

Mkoa wa Rukwa katika tathmini ya lishe iliyofanyika jijini Dodoma Septemba 30 mwaka huu ilitangazwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa kwa utekelezaji mzuri wa afua za lishe.

Mwisho

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa