• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Miradi ya ULGSP yawa kivutio kwa wageni katika mji wa Sumbwanga

imewekwa Tar: June 2nd, 2020

Katika kuhakikisha maendeleo ya nchi yanamgusa kila mwananchi katika mikoa, Wilaya na Halmashauri nchini, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) imepewa dhamana ya kusimamia programu ya uimarishaji miji (Urban Local Government Support Program – ULGSP) kwaajili ya kuimarisha halmashauri 18 za miji na manispaa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Hivi karibuni (2.6.2020) Waziri wa OR – TAMISEMI Mh. Suleiman Jafo ametembelea miradi mitatu inayotekelezwa na program ya ULGSP yenye thamani ya Shilingi 26,998,770,878.66/= ambapo alikagua mradi wa Kituo cha Malori kilichopo Utengule kata ya Lwiche, kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Mabasi kilichopo Katumba Azimio kata ya Pito pamoja na kuzindua mradi wa barabara za kilometa 11.577 zilizozunguka katika mitaa kadhaa ya mji wa Sumbawanga.

Katika kusifia mabadiliko ya mji wa Sumbawanga kutokana na utekelezwaji wa miradi hiyo Mh. Jafo alisema kuwa Sumbawanga ya miaka mitano iliyopita siyo Sumbawanga ya sasa kwani barabara zilizotapakaa katika mji huo zimeng’arisha mji na hivyo kuwapongeza wanasumbawanga kwa kuwa na mji unaovutia na kuwatanabahisha kuwa kuna miji ambayo inatamani kuwa na barabara kama hizo lakini hawana.

“Barabara zilizofungwa na mataa, tena barabara zenu sio za ‘Double Surface Dressing’ sio barabara za Lami nyepesi hapana, mmepata barabara zilizotengenezwa na lami nzito, wanasumbawanga mnabahati sana sana, katika watu ambao Mheshimiwa Rais amewapendelea wapate mafanikio makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara ni watu wa manispaa ya Sumbawanga, barabara zenu ikifika usiku ni kama utalii, mji wa sumbawanga usiku unameremeta,” Alisema.

Na kuongeza kuwa hapo zamani watumishi wengi wa serikali walikuwa wanagoma kupangiwa Sumbawanga tofauti na sasa ambapo mji umependeza na watumishi waliopo hawatamani kuondoka, kwa kuwa mji huo umekuwa wa kitalii kwa wageni wanaoingia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipokuwa akisoma taarifa ya mkoa kwa Waziri huyo alisema kuwa, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga inatarajia kutekeleza programu ya TACTIC (Tanzania, Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness) utakaosimamiwa na OR – TAMISEMI utakaofadhiliwa na Benki ya Dunia, ukitarajiwa kuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 35.26.

“Katika programu hii mradi mbalimbali inatarajiwa kutekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 35.26 ambayo ni ujenzi wa Soko la Mazao eneo la Kanondo, Ujenzi wa Dampo la Kisasa kule Mbalika na ujenzi wa barabara zenye urefu wa Km. 13, barabara hizo zitakuwa kwa kiwago cha lami, ile lami ya Zege inayoitwa ‘Asphalt Concrete’. Ni matarajio yetu kuwa fedha hizo zitakuja kwa wakati ili tuweze kutekeleza miradi hiyo kwa haraka,” Alisema.

Awali wakati akitoa taarifa ya miradi hiyo ya ULGSP Mratibu wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijiji (TARURA) Mhandisi Suleiman Mziray alieleza madhumuni ya miradi hiyo kuwa ni kuhakikisha halmashauri inaongeza vyanzo vya mapato, kuongeza fursa za biashara kwa wananchi wanaoishi karibu na miradi hiyo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kama migahawa, maduka na nyumba za kulala waeni na hivyo kuongeza ajira na kipato cha mwananchi mmoja mmoja.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa