• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Miradi ya ULGSP yawa kivutio kwa wageni katika mji wa Sumbwanga

imewekwa Tar: June 2nd, 2020

Katika kuhakikisha maendeleo ya nchi yanamgusa kila mwananchi katika mikoa, Wilaya na Halmashauri nchini, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) imepewa dhamana ya kusimamia programu ya uimarishaji miji (Urban Local Government Support Program – ULGSP) kwaajili ya kuimarisha halmashauri 18 za miji na manispaa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Hivi karibuni (2.6.2020) Waziri wa OR – TAMISEMI Mh. Suleiman Jafo ametembelea miradi mitatu inayotekelezwa na program ya ULGSP yenye thamani ya Shilingi 26,998,770,878.66/= ambapo alikagua mradi wa Kituo cha Malori kilichopo Utengule kata ya Lwiche, kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Mabasi kilichopo Katumba Azimio kata ya Pito pamoja na kuzindua mradi wa barabara za kilometa 11.577 zilizozunguka katika mitaa kadhaa ya mji wa Sumbawanga.

Katika kusifia mabadiliko ya mji wa Sumbawanga kutokana na utekelezwaji wa miradi hiyo Mh. Jafo alisema kuwa Sumbawanga ya miaka mitano iliyopita siyo Sumbawanga ya sasa kwani barabara zilizotapakaa katika mji huo zimeng’arisha mji na hivyo kuwapongeza wanasumbawanga kwa kuwa na mji unaovutia na kuwatanabahisha kuwa kuna miji ambayo inatamani kuwa na barabara kama hizo lakini hawana.

“Barabara zilizofungwa na mataa, tena barabara zenu sio za ‘Double Surface Dressing’ sio barabara za Lami nyepesi hapana, mmepata barabara zilizotengenezwa na lami nzito, wanasumbawanga mnabahati sana sana, katika watu ambao Mheshimiwa Rais amewapendelea wapate mafanikio makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara ni watu wa manispaa ya Sumbawanga, barabara zenu ikifika usiku ni kama utalii, mji wa sumbawanga usiku unameremeta,” Alisema.

Na kuongeza kuwa hapo zamani watumishi wengi wa serikali walikuwa wanagoma kupangiwa Sumbawanga tofauti na sasa ambapo mji umependeza na watumishi waliopo hawatamani kuondoka, kwa kuwa mji huo umekuwa wa kitalii kwa wageni wanaoingia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipokuwa akisoma taarifa ya mkoa kwa Waziri huyo alisema kuwa, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga inatarajia kutekeleza programu ya TACTIC (Tanzania, Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness) utakaosimamiwa na OR – TAMISEMI utakaofadhiliwa na Benki ya Dunia, ukitarajiwa kuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 35.26.

“Katika programu hii mradi mbalimbali inatarajiwa kutekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 35.26 ambayo ni ujenzi wa Soko la Mazao eneo la Kanondo, Ujenzi wa Dampo la Kisasa kule Mbalika na ujenzi wa barabara zenye urefu wa Km. 13, barabara hizo zitakuwa kwa kiwago cha lami, ile lami ya Zege inayoitwa ‘Asphalt Concrete’. Ni matarajio yetu kuwa fedha hizo zitakuja kwa wakati ili tuweze kutekeleza miradi hiyo kwa haraka,” Alisema.

Awali wakati akitoa taarifa ya miradi hiyo ya ULGSP Mratibu wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijiji (TARURA) Mhandisi Suleiman Mziray alieleza madhumuni ya miradi hiyo kuwa ni kuhakikisha halmashauri inaongeza vyanzo vya mapato, kuongeza fursa za biashara kwa wananchi wanaoishi karibu na miradi hiyo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kama migahawa, maduka na nyumba za kulala waeni na hivyo kuongeza ajira na kipato cha mwananchi mmoja mmoja.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa