• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Miundombinu ikiimarishwa hakika viwanja vya nambogo vitajiuza vyenyewe,” RC Wangabo.

imewekwa Tar: March 13th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemshauri Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga kuhakikisha anakamilisha miundombinu ya barabara na mahitaji muhimu katika mradi wa upimaji viwanja katika Kijiji cha Nambogo ili kuwavutia wanunuzi na matokeo yake kupata wateja kwa haraka kuliko hali ilivyo sasa.

“Miundombinu mbalimbali mkaisogeza, huduma za maji, umeme, kunajiuza kwenyewe, hapa ni karibu na barabara na kuko bize kwenda Mbeya kuliko upande huu wa kwenda Mpanda, hakikisheni mnaweka vibanda vya biashara na kituo cha basi na mhakikishe kuwa kituo hicho kinafanya kazi basi hivi viwanja vitajiuza vyenyewe na havitatosha, hivyo cha kwanza kuhakikisha miundombinu ya msingi ipo kisha patajiuza penyewe,” Alisisitiza.

Mradi huo wenye jumla ya viwanja 2161 vilivyopimwa katika eneo la Nambogo na Katumba Azimio vimetengwa maalum kwa matumizi mbalimbali ikiwemo makazi, biashara, shule, huduma za afya, maofisi, “Shopping Mall”, vituo vya mafuta, viwanja vya michezo na maeneo ya kupumzikia. Mradi ambao tayari umeshagharimu Tsh. 1,589,692,000.

Afisa Ardhi manispaa ya Sumbawanga Thadeo maganga amesema kuwa lengo la mradi huo ni kuwa mji wa kisasa utakaokuwa na huduma mbalimbali ili kupunguza msongamano wa kufuata huduma katika eneo la kitovu cha mji kwa siku za usoni na kuonheza upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa na kuwekewa miundombinu ya msingi na hivyo kupunguza kasi ya ujenzi holela.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbwanga amesema kuwa tayari wameshaanza kupokea maombi ya mahitaji ya viwanja hivyo na kuwataka wananchi kuendelea kujitokeza ili kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba kwa maeneo hayo mapya na kuweza kutanua mji huku akibainisha juhudi zinazofanyika za kuongea na benki ya NMB kwaajili ya kuwakopesha wananchi ili waweze kumudu ununuzi wa viwanja hivyo.

“hapa tunazungumzia viwanja 2161 ni mradi mkubwa ambao NMB wanaweza wakakopesha, tupo katika mijadala ya awalai ambapo tunataka “tu-twist” sheria yao “wanayo-mortgage” mpango wa ujenzi, lakini lazima uwe umeshaanza kujenga, ila si tunawaambia hawa hawajaanza lakini waone jinsi gani ambavyo wanaweza, tunawasiliana makao makuu kama wataiona hii ni fursa ya waombaji 2000 ambao tunaweza tukaingia nao mkataba mdogo na NMB ili waweze kuwakopesha wanunue wakwatwe polepole ili kuufanya huu mji uwende kwa kasi,” Alimalizia.

Jumla ya viwanja 1997 vitauzwa kwa bei elekezi ambapo kwa kila mita moja ya mraba kwa makazi pekee ni 2,700/=, makazi na biashara 3,000/=, biashara 5,000/=, huduma za jamii 3,500/=, ibada/kuabudu 3,500/=, hoteli, vituo vya mafuta na maduka ya kiuwekezaji 5,000/=.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa