• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mkandarasi atakiwa kumaliza Jengo la Ofisi za Halmashauri kabla ya 2021.

imewekwa Tar: December 12th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkandarasi Suma JKT anayejenga Ofisi za halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kumaliza jengo hilo kabla ya mwaka mpya wa 2021 baada ya jengo hilo kudumu kwa miaka zaidi ya mitatu bila ya kukamilika.

Mh. Wangabo amesema kuwa Pamoja na kufahamu changamoto kadhaa za ujenzi zilizoikumba eneo hilo hali iliyofanya ujenzi wa msingi wa jengo hilo kuchukua muda mrefu kutokana na eneo hilo kujaa maji na hivyo mkandarasi kuomba kuongezewa muda wa kumalizia jengo hilo lakini ameongeza kuwa hatua hiyo imeshapita.

“Mkandarasi aliomba ‘extension’ kadhaa nay a mwisho inaisha tarehe 31 Disemba yam waka huu, sasa nikuangize mkandarasi uzingatie huo mkataba, mkataba huo wa tarehe hiyo niliyoisema ufuatwe, kazi zifanyike usiku na mchana, leo ni tarehe 11 bado kama wiki tatu, hili jingo linapaswa kukamilika vinginevyo tutatafakari hatua ya kuchukua kwasababu tumeshakaa muda mrefu miaka mitatu haikubaliki,” Alisema.

Aidha, alitahadharisha kuwa fedha inayotolewa kwaajili ya ujenzi wa jingo hilo kutumika kwaajili ya malengo ya ujenzi wa jingo hilo na sio badala yake Mkandarasi huyo kubadili matumizi ya fedha hizo kutokana na taratibu zao za kuweka fedha za miradi yao sehemu moja na hatimae kubadili matumizi.

Hata hivyo wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi huo mshauri elekezi Kaimu Meneja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Rukwa Mhandisi Haruna Kalunga amesema kuwa miongoni mwa changamoto wanazopata ni Pamoja na mshitiri kuchelewa kufanya malipo kwa wakati hali inayosababisha ucheleshwaji wa ujenzi huo.

“Kwa mfano hati ya madai namba 5 ilipitishwa na Mshauri Elekezi tarehe 5.6.2020 ila ilikuja kulipwa tarehe 5.10.2020 takriban miezi minne mkandarasi alikuwa anasubiria malipo, changamoto ya pili ni kuchelewa kupatikana kwa mkandarasi mdogo wa huduma, mpaka unaona jingo hili linaanza kutumika hadi leo halina miundombinu ya umeme,” Alieleza.

Ujenzi huo wenye thamani ya Shilingi 3,494,444,696/= unaojumuisha ujenzi wa vymba vya ofisi 137, jingo la mgahawa, uzio wa mita 427, kibanda cha mlinzi na maegesho ya magari ulianza tarehe 27.10.2017 na kutarajiwa kumalizika tarehe 25.5.2019 lakini hadi leo tarehe 11.12.2020 umefikia 56% huku mkandarasi akiwa amelipwa hati 5 za madai zenye jumla ya shilingi 1,869,535,687.55/= ambazo ni saw ana 45% ambapo gharama hizo ni bila ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT).

Katika Hatua nyingine Mh. Wangabo amepongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa kutumia fedha zake za mapato kuendelea na ujenzi wa ofisi za halmshauri hizo wakati wakisubiri fedha kutoka serikalini lakini pia kuanzisha ujenzi wa Stendi ya Mabasi katika mji mdogo wa Laela ambao ndio makao makuu mapya ya Halmashauri hiyo baada ya agizo la Rais Mh. John Pombe Magufuli kuzitaka halmashauri hizo kuhamia katika maeneo yao ya kiutawala.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa