• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mkandarasi wa REA Mkoani Rukwa kukataliwa kuendelea na mradi.

imewekwa Tar: March 1st, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesisitiza kukataliwa kuendelea na utekelezaji Mradi wa Mmeme Vijiji (REA) mkandarasi Nakuroi Investment kwa kushindwa kufikia hata nusu ya utekelezaji wa mradi huo hadi kufikia mwezi Februari mwaka huu.

Mkandarasi huyo ambaye alitegemewa kutekeleza mradi huo katika vijiji 111 vya mkoa wa Rukwa tangu mwezi Novemba mwaka 2017 aliposaini mkataba na kumalizika mwezi June mwaka 2019 huku akiwa amekamilisha mradi katika vijiji 23 tu hadi kufikia februari mwaka 2019.

“itakapofika mwezi June huenda hata robo tutakuwa hatujafika, kwa hali hii niseme tu wazi huyu Mkandarasi Nakuroi Investment mimi naona uwezo wake ni mdogo lakini pia eneo amepewa ni kubwa sana huyu anashughulikia Mkoa mzima vijiji tulivyonavyo ni 339 mkoani kwetu, hap ani lazima wizara ifanye kitu, mi niseme tu wazi kuwa ikifika mwisho wa mkataba wake hatutamkubali tena kuendelea na mkataba mwingine, watuongezee wakandarasi, tunahitaji kupata umeme katika vijiji vyetu vyote kwa mujibu wa mkataba,” Mh. Wangabo Alisisitiza.

Kauli hiyo imetoka wakati wa majadiliano juu ya kusuasua kwa utekelezaji wa mradi REA katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo katika mkoa ambapo hoja hiyo iliwasilishwa kutoka katika maazimio ya kikao cha kamati ya ushari ya Wilaya ya Sumbawanga iliyowasilishwa katika kikao hicho.

Kwa upande wake Kaimu meneja wa TANESCO Mkoani Rukwa Gilles Daniel alikiri kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo huku akieleza changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo ili kuhakikisha maagizo ya serikali yanatekelezwa kwa wakati na wananchi wote wanapata umeme ambao serikali imewaahidi.

Alisema kuwa changamoto kubwa imekuwa ni upatikanaji wa vifaa kwaajili ya mradi jambo lililosababishwa na uzalishaji mdogo wa vifaa hivyo kwenye viwanda vya ndani na pia kukosa ubora unaotarajiwa.

“umeme umewashwa katika vijiji 23 tu peke yake, ni kweli kwamba mradi unasuasua hatujaenda kwa kasi ile ambayo inatakiwa kwasababu ya changamoto nyingi ambazo zimetokea zinazosababisha mradi kusuasua lakini ni juzi tu waziri alitoa maagizo ya kuwashwa vijiji vitatu kwa kila Wilaya na utekelezaji umeanza na ndani ya siku mbili umeme utakuwa yumewashwa ndani ya vijiji vitatu kila wilaya,” alisema.

Akitetea hoja hiyo Mbunge wa Sumbawanga Mjini Mh. Aeshi Hilaly amesema kuwa si vyema kuwatwisha mzigo huo Shirika la Umeme na hivyo ni jukumu la waheshimiwa wabunge wa mkoa wa Rukwa kwa ushirikiano kulichukua hilo na kulifikisha bungeni ili kulipatia ufumbuzi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa