• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MKUU WA MKOA WA RUKWA ATOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

imewekwa Tar: October 27th, 2025


Na Khadija Dalasia, Rukwa


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere, ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Ametoa wito huo leo, Oktoba 27, 2025, akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, mshikamano na utulivu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa mafanikio.


Kwa mujibu wa Ibara ya 5 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2024, kila raia mwenye sifa kisheria ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali za uongozi.


Mheshimiwa Makongoro amesema Serikali imeweka mazingira wezeshi kuhakikisha wananchi wote wanapata fursa ya kushiriki katika uchaguzi huo kwa uhuru, usalama na amani. Aidha, amebainisha kuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametangaza tarehe 29 Oktoba 2025 kuwa siku ya mapumziko ya kitaifa ili kutoa nafasi kwa wananchi wote kushiriki kikamilifu katika kupiga kura.


Amehimiza wananchi wa Rukwa kufika vituoni mapema siku ya uchaguzi wakiwa na vitambulisho vyao vya mpigakura, kufuata maelekezo ya maafisa wa uchaguzi na vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga utulivu na amani katika jamii.


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga ipasavyo kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira salama na ya utulivu katika maeneo yote ya Mkoa wa Rukwa.


Aidha, amekumbusha wananchi kuwa uchaguzi ni nyenzo muhimu ya maendeleo na sio chanzo cha migawanyiko, hivyo amewataka kuendelea kudumisha umoja na mshikamano baada ya uchaguzi. Ameongeza kuwa wananchi wanapaswa kuutumia uchaguzi kama fursa ya kuchagua viongozi bora watakaosimamia maendeleo ya Taifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.


Kwa ujumla, wito huo umetolewa ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni za uhamasishaji wa wananchi kote nchini kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa amani, umoja na uzalendo.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKUU WA MKOA WA RUKWA ATOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 27, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI RUKWA LAPOKEA MAGARI MATATU YA KISASA KUIMARISHA SHUGHULI ZA UOKOAJI

    October 27, 2025
  • SERIKALI YATOA PIKIPIKI KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WA HALMASHAURI RUKWA

    October 24, 2025
  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa