• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MPANGO BORA WA UFUGAJI NYUKI WAWAFIKIA MACHIFU RUKWA

imewekwa Tar: August 20th, 2025


Na Khadija Dalasia - Rukwa, Agosti 2025

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) imewakabidhi zaidi ya mizinga 200 ya kisasa ya nyuki kwa Machifu wa Mkoa wa Rukwa ikiwa sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa kuendeleza Sekta ya Ufugaji Nyuki ujulikanao kama “Achia Shoka, Kamata Mzinga”.

Akikabidhi mizinga hiyo kwa Machifu wa Wilaya ya Sumbawanga, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii anayeshughulikia Uhifadhi, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba, alisema mpango huo unalenga kuongeza uzalishaji wa asali nchini kutoka tani 33,861 za sasa hadi tani 75,000 ifikapo Juni 2035.

“Ugawaji huu unaunga mkono juhudi za Mhifadhi namba moja nchini, Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuwainua wananchi kiuchumi kupitia uhifadhi wa maliasili hususan misitu na nyuki,” alisema CP. Wakulyamba.

Aidha, aliwataka Machifu na wananchi kushirikiana na wataalam wa Wizara katika kujifunza mbinu za kisasa za ufugaji nyuki na kuhakikisha rasilimali hizo zinahifadhiwa kwa vizazi vijavyo. Pia aliitaka TFS kuimarisha ulinzi wa maeneo ya hifadhi na kuendeleza shughuli za utalii.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Msalika Makungu, alisema kwa sasa mkoa una jumla ya mizinga ya kisasa 5,710, mizinga ya kienyeji 2,251 na wafugaji 3,736, hivyo mizinga hiyo mipya itaongeza tija katika sekta ya ufugaji nyuki.

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara hiyo, Daniel Pancras, alibainisha kuwa sekta ya ufugaji nyuki inachangia ajira takribani milioni 2 nchini kupitia uzalishaji, uchakataji na biashara ya asali pamoja na vifaa vya kufugia nyuki.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa