• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mwenge wa Uhuru 2021

imewekwa Tar: September 21st, 2021

MIRADI YA BILIONI 10 KUTEMBELEWA NA MWENGE WA UHURU MKOANI RUKWA

MWENGE wa Uhuru Kitaifa utatembelea miradi 18 ya maendeleo na vikundi saba vya wajasiriamali mkoani Rukwa kwa pamoja vikiwa na thamani ya Sh bilioni 10.55/-

Miradi hiyo itawekewa mawe ya msingi, itakaguliwa na kuzinduliwa katika wilaya tatu za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa,Joseph Mkirikiti alieleza hayo jana (20.09.2021)  baada ya kukabidhiwa mwenge  huo na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Omary Mgumba katika sherehe ya makabidhiano katika kijiji cha Tunko kilichopo katika wilaya ya Sumbawanga mpakani na Mkoa wa Songwe.

Akizungumzia mchanganuo wa uchangiaji wa miradi hiyo alisema wananchi wamechangia Sh 101,496,100.00, Halmashauri zimechangia Sh 183,094,374/-, Serikali Kuu umechangia Sh 9,986,485,860/- huku wadau wa maendeleo na wahisani wamechangia Sh 286,174,244.07

" Mwenge wa Uhuru Kitaifa utakimbizwa kilomita 544.9 katika wilaya tatu za kiutawala" alieleza.

Alisema mkoa umejipanga kikamilifu katika kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru 2021 " TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu ; Itumike kwa usahihi na uwajibikaji".

Akizungumzia mapambano dhidi ya rushwa alisema katika kipindi cha Juni2020 hadi Julai 2021 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa uliokoa kiasi cha Sh 502,952,380/- ambazo Sh 334,464,330/- zilidhibitiwa na Sh 168,488,000/- zilikuwa fedha taslimu.

Kwa upande wake Kiongozi wa Taifa wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Luteni Josephine Mwambashi alizitaka halmashauri kuhakikisha nyaraka zote muhimu zinakuwepo katika miradi itakayokaguliwa.

Pia alizitaka halmashauri katika miradi yote itakayokaguliwa na mwenge huo wawepo wataalamu ambapo watatoa taarifa za kina pia wawe na uwezo wa kujibu maswali watakayoulizwa na wakimbizi Mwenge Kitaifa.

Ukiwa katika halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga Mwenge wa Uhuru umezinduka jengo la ofisi ya Mthibiti Ubora wa Elimu katika mji mdogo wa Laela ambalo ujenzi wake umegharimu zaidi ya Sh milioni 169.2/- na

Pia utazindua vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu katika Shule ya Sekondari Sumbawanga ambao ujenzi wake umegharibu Sh milioni 44/- na utakagua barabara ya Mpanda 'Road' - Katandala Mission- Mashine za Mpunga- Majengo ambao ujenzi wake umegharimu Sh bilioni 7.9/-

Mwenge wa Uhuru ulioasisiwa na Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1961 mbio zake zilianza rasmi mwaka 1964 huu ukiwa ni mwaka 29 tangu mbio za Mwenge wa Uhuru zirejeshwe chini ya uratibu na usimamizi wa Serikali

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa