• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mwenge wa Uhuru waacha maumivu kwa Ma-DC – Rukwa

imewekwa Tar: April 11th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku tatu kwa wakuu wa wilaya wanaosimamia halmashauri ambazo Mwenge wa Uhuru umekataa kuweka mawe ya msingi au kuzindua miradi iliyopitiwa na Mwenge huo kutoa maelezezo ya kina juu ya sababu ya kukataliwa kwa miradi hiyo yenye tamani ya shilingi 1,248,489,871.

“Napenda nitoe maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya wenye miradi iliyokataliwa kunipa taarifa ya kwanini miradi yao haikuzinduliwa/kuwekewa mawe ya msingi. Maelezo hayo niyapate ndani ya siku tatu kuanzia tarehe ya leo hadi tarehe 14, April, 2019,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo muda mfupi kabla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Amos Makalla huku Mwenge huo ukiwa umekimbizwa katika halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa zikichukua umbali wa kilemeta 832.5 na kutembelea miradi 35 na vikundi 11 ikiwa na tamani ya shilingi 45,404,104,489.59

Aidha, kutokana na mbio hizo za Mwenge wa Uhuru kubeba kauli mbiu isemayo “Maji ni haki ya Kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa,” hivyo alitoa wito kwa wananachi kuendela kutunza vyanzo vya maji, kuimarisha jumuia za watumia maji pamoja na kufanya maandalizi thabiti ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo.

Kwa upande wake Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2019 Ndugu Mzee Mkongea Ali aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Rukwa kwa kumpa ushirikiano wa Kutosha tangu wanawasili katika mkoa huo hadi kuondoka na kuelekea katika mkoa wa Katavi na kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa kufikisha asilimia 55 ya wananchi wa Mkoa huo kupata maji safi na salam.

“Mimi nikupe hongera kwasababu takwimu zinaonyesha katika mkoa wako wa Rukwa umejitahidi kwa asilimia 55 kuhakikisha wananchi woyte wanapata maji ya uhakika na salama sambamba na hilo katika kupambana na Rushwa katika TAKUKURU kuna malalamiko 64 na kesi 59 wanazifanyia kazi, endeleeni kufanya kazi na kuhakikisha haki inapatikana kwa wote,” Alisema.

Kutokana na mapungufu yaliyobainika Mwenge wa Uhuru haukuzindua amakuweka mawe ya msingi kwenye miradi mitatu, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga mradi mmoja vyumba vitano vya madarasa wenye thamani ya shilingi 76,250,000, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mradi mmoja wa ujenzi wa nyumba ya waalimu “6 in 1” wenye thamani ya shilingi 174,977,775 na Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo mradi mmoja wa maji wenye thamani ya shilingi 997,262,096.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa