• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI WILAYANI NKASI; KIONGOZI ATAKA WANANCHI WATUMIE FURSA YA ELIMU YA UFUNDI

imewekwa Tar: September 28th, 2025



Mwenge wa Uhuru 2025 ukiwa katika siku yake ya kwanza mkoani Rukwa, umeweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali wilayani Nkasi, hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa elimu ya ufundi kwa vijana.

Akizungumza katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi leo Septemba 28, 2025, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndg. Ismail Ali Ussi, amewataka wazazi na walezi kuwahamasisha watoto wao kusoma katika shule za amali ili kupata ujuzi wa vitendo utakaowawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.


Kiongozi huyo ametumia fursa hiyo kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mheshimiwa Peter Ambrose Lijualikali, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Bw. Afraha Nassoro Hassan, kwa kusimamia vyema utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa maendeleo ya wananchi.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa kukamilisha ujenzi wa shule hiyo kwa wakati ili ianze kutoa huduma kwa vijana waliokusudiwa ili kuleta mageuzi katika sekta ya elimu ya ufundi mkoani Rukwa.

Katika hatua nyingine, Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Ndg. Ismail Alli Ussi amewapongeza wananchi wa Nkasi kwa ushiriki wao wa moja kwa moja katika shughuli za maendeleo, akieleza kuwa mshikamano huo unaonyesha dhamira ya kweli ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.


Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuendelea na mbio zake kesho tarehe 29 Septemba 2025, kwa kukabidhiwa rasmi kwa Manispaa ya Sumbawanga, ambapo utaendelea kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo kabla ya kuelekea Halmashauri za Wilaya za Kalambo na Sumbawanga.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MANISPAA YA SUMBAWANGA, MIRADI YA BILIONI 30.3

    September 29, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI WILAYANI NKASI; KIONGOZI ATAKA WANANCHI WATUMIE FURSA YA ELIMU YA UFUNDI

    September 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOANI RUKWA; KUKIMBIZWA KWA SIKU NNE; KUMULIKA MIRADI YA BILIONI 55.3

    September 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa