• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Naibu Waziri Mabula Aipa NHC Miezi Mitano Kukamilisha Mradi Wa Ujenzi Nyumba Za Makazi Sumbawanga

imewekwa Tar: January 23rd, 2020

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuhakikisha inakamilisha mradi wake wa ujenzi wa nyumba za Makazi za Jangwani katika Manispaa ya Sumbawanga mkoa wa Rukwa katika kipindi cha mwaka huu wa fedha 2019/2020.


Akizungumza wakati akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba hizo za makazi wenye jumla ya nyumba ishirini za ghorofa moja jana katika Manispaa ya Sumbawanga mkoa wa Rukwa Naibu Waziri Mabula alisema mradi huo lazima ukamilishwe mapema kwa kuwa fedha iliyotumika ni nyingi.


Kauli hiyo ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inafuatia kuelezwa na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo kuwa mradi huo umekuwa ukimsumbua kutokana na kuchukua muda mrefu bila kukamilika na hivyo kuufanya mkoa kutojua hatma yake wakati uhitaji wa nyumba za kupanga katika manispaa ya Sumbawanga ni mkubwa.


‘’ Naungana na RC kuwa mradi huu umechukua muda mrefu hivyo ni lazima uishe katika mwaka huu wa fedha wa kiserikali na April mwaka huu 2020 narudi hapa Sumbawanga’’ alisema Dkt Mabula.


Kwa mujibu wa Meneja Mawasiliano wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Muungano Saguya, mradi huo wa ujenzi wa nyumba za Makazi Jangwani katika Manispaa ya Sumbawanga ulianza mwezi Juni 2014 na ulisimama kupisha uchunguzi baada ya kuwepo tuhuma za ubadhilifu kwenye mradi huo.


Hata hivyo, Saguya alisema kiasi cha shilingi milioni 366.2 kinahitahika kumalizia mradi huo na tayari Shirika lake limejipanga na maandalizi kwa ajili ya ukamilishaji mradi yamekamilika na muda wowote umaliziaji nyumba hizo utaanza.


Mradi huo wa Nyumba za Makazi Jangwani katika Manispaa ya Sumbawanga mkoa wa Rukwa ambao nyumba moja ilishanunuliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHF) zikikikamilika zitapangishwa na zitaweza kuliingizia Shirika la Nyumba la Taifa kiasi cha shilingi 5,400,000 kila mwezi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa