• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

NFRA

imewekwa Tar: May 11th, 2022

DOLA MILIONI 6 ZAKAMILISHA UJENZI WA VIHENGE VYA KISASA SUMBWANGA

Na. OMM Rukwa

Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kanda ya Sumbawanga imefanikisha ujenzi wa vihenge nane na ghala moja la kisasa vitakavyoongeza uwezo wa kuhifadhi mazao tani 25,000 kwa gharama ya Dola za Kimarekani Milioni 6.019.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti aliyetembelea mradi huo uliopo eneo la Kanondo katika Manispaa ya Sumbawanga alisema kukamilika kwake ni mafanikio kwa wakulima wa Rukwa na Taifa kuwa na uwezo wa kuhifadhi nafaka kisasa.

“Mradi huu utakuwa mkombozi kwa Taifa kuhifadhi akiba yake ya chakula kwa njia ya kisasa ambapo wananchi wa Rukwa ndio wanufaika wakubwa kutokana na vihenge hivi kuwa hapa Sumbawanga” alisema Mkirikiti.

Akitoa taarifa ya mradi huo , Mhandisi Mkazi toka kampuni ya M/s Unia Araj  ya Poland Mhandisi Haruna Kalunga alisema mradi huu ulianza kutekelezwa mwaka 2020 umehusisha ujenzi wa vihenge nane, majengo 6,ghala moja, mzani mmoja na uzio  kuzunguka eneo hilo.

Mhandisi Kalunga aliongeza kusema vihenge hivyo vya kisasa vikubwa vipo sita na vidogo viwili pamoja na miundombinu yake vina uwezo wa kubeba tani 20,000 ambapo ghala la kuhifadhia mazao limekamika pia likiwa na uwezo wa kubeba tani 5,000  na kuwa mradi huo umekamilika mwezi Machi mwaka huu na majaribio tayari yamefanyika mwezi Aprili mwaka huu.

“Mpaka sasa mkandarasi ameshalipwa Dola za Kimarekani 5,417,459 sawa na asilimia 90 ya fedha zote za mkataba ambazo ni Dola za Kimarekani 6,019,399” alieleza Mhandisi Kalunga.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kalunga alitoa ombi kwa serikali kupitia VETA kuwarasimisha vijana wa kitanzania wapatao 60 ambao walioshiriki kazi za ujenzi wa vihenge vyote na miundombinu yake kutokana na uwezo na uzoefu wao.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tunaomba vijana wazalendo walioshiriki ujenzi wa mradi huu warasimishwe na VETA kupitia mpango wa urasimishaji ujuzi nje ya mfumo rasmi” alihitimisha taarifa yake Mhandisi Kalunga.

Naye Meneja wa NFRA Kanda ya Sumbawanga Marwa Range alisema kufuatia kukamilika kwa mradi huo Wakala tayari umeanza kutumia miundombinu hiyo kuhifadhi mazao na kuwa utasaidia kuboresha hali ya uhifadhi nafaka kwa matumizi ya Taifa.

Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kupitia mpango wa Storage Capacity Expansion Project (SCEP) ilipokea mkopo wa fedha wenye masharti mepesi toka serikali ya Poland kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa vihenge vya kuhifadhia mazao na miundombinu yake kwenye mkoa wa Rukwa.

Mwisho.

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chanjo Polio

    May 18, 2022
  • NFRA

    May 11, 2022
  • Vyama vya Ushirika

    May 05, 2022
  • Eng. Kundo: Nimeridhishwa na Zoezi la Anwani za Makazi Rukwa

    April 27, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa