• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Rais Magufuli aanza Ziara Mkoani Rukwa

imewekwa Tar: October 6th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amezindua barabara ya Tunduma – Laela – Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 223.2 ambayo ni sehemu ya barabara kuu katika ushoroba wa magharibi unaoanzia Tunduma – Mpanda – Kigoma – Nyakanazi wenye urefu wa kilometa 1,286.

Ujenzi wa barabara hiyo umegharimu shilingi Bilioni 373 na Milioni 949 kwa ufadhili wa mfuko wa changamoto za milenia (MCC) na kukamilika kwake kumesaidia kuinua shughuli za kiuchumi katika ukanda wa nyanda za juu kusini na ukanda wa magharibi, na pia kumeunganisha usafiri kati ya Tanzania na nchi jirani za Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi, Rwanda na Uganda.

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa barabara hiyo zilizofanyika katika Mji Mdogo wa Laela Wilayani Sumbawanga, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Mikoa yote inayonufaika na barabara hiyo na amewahakikishia kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati ya kuhakikisha barabara kuu zote za ukanda wa magharibi zinajengwa kwa kiwango cha lami.

Ameishukuru Marekani kupitia MCC kwa ufadhili wa mradi huo, Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa mradi huo kutekelezwa katika kipindi chake na ameipongeza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa usimamizi wa ujenzi wa barabara hiyo, na pia amewataka wananchi na watumiaji wa barabara hiyo kutunza miundombinu yake kwa kutochimba mchanga kando ya barabara na madaraja, kutomwaga mafuta barabarani na kutoiba alama za barabarani.

Katika mkutano huo, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kuchukizwa na taarifa za kuchomwa moto mitambo ya umeme jua ya mradi wa maji wa Mji Mdogo wa Laela uliogharimu shilingi Bilioni 1.7 na ameagiza waliohusika kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Aidha, baada ya kupokea malalamiko dhidi ya mkandarasi Fally Enterprises Ltd aliyepatiwa zabuni ya kujenga mradi huo pamoja na miradi mingine ambayo inadaiwa kutofanya kazi kama ilivyotarajiwa licha fedha zake kulipwa, Mhe. Rais Magufuli ametoa siku 7 kwa vyombo vya dola kumkamata, kuchunguza na kumfikisha katika vyombo vya sheria, na pia ameiagiza Wizara ya Maji kuwachunguza na kuwachukulia hatua za kisheria maafisa wote wa wizara waliohusika kumpa zabuni mkandarasi huyo.

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kuchukizwa na taarifa ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola juu ya Askari Polisi 9 waliokuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa na kuwabambikiza kesi wananchi, na amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP-Simon Sirro kumsimamisha kazi Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Sumbawanga ACP-Polycarp Urio kwa kutowasilisha taarifa ya maelekezo ya Waziri Lugola aliyeagiza Askari Polisi hao wahamishwe kituo cha kazi.

Pia, Mhe. Rais Magufuli ametoa mwezi 1 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ambayo ofisi zake zipo Sumbawanga Mjini kuhamia katika Mji Mdogo wa Laela ili kutoa huduma jirani na wananchi na ameelekeza kuwa mtumishi yeyote ambaye hatatii agizo hilo afukuzwe kazi mara moja.

Sambamba na agizo hilo, Mhe. Rais Magufuli ametoa mwezi 1 kwa ofisi zote za taasisi za umma zilizopo kwenye majengo ya kupanga, kuhamia katika majengo ya Serikali ili kuokoa fedha za Serikali ambazo zimekuwa zikitumika kulipia gharama za kupanga katika majengo yasiyo ya Serikali.

Kwa TANROADS Makao Makuu ambayo ofisi zake zipo katika jengo la kupanga lililopo Morocco Jijini Dar es Salaam, Mhe. Rais Magufuli ametoa siku 5 kwa ofisi hizo kuhamia katika majengo ya Serikali.

Akiwa njiani kutoka Tunduma Mkoani Songwe kwenda Sumbawanga Mkoani Rukwa, Mhe. Rais Magufuli amesimama kuwasalimu wananchi wa Vijiji vya Chiwanda, Ndalambo, Ikana na Lwasho Wilayani Momba, na Vijiji vya Ikosi, Mpui, Kaengesa, Mkonda na Tamasenga Wilayani Sumbawanga ambako amewataka kutumia uwepo wa barabara nzuri ya lami kuongeza uzalishaji wa mazao kwa kuwa sasa wana uhakika wa kuyafikia masoko ya ndani na nje ya nchi.

Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mawaziri amesema Serikali imechukua hatua madhubuti za kuhakikisha Watanzania wanapata umeme, elimu bila malipo, wanaboreshewa huduma za matibabu na kwamba pamoja kuimarisha zaidi huduma hizo, imeanza kushughulikia tatizo la maji ambalo linayakabili maeneo mengi ikiwa ni pamoja kuwashughulikia wakandarasi na maafisa wa Serikali wanaohujumu miradi hiyo.

Kesho tarehe 07 Oktoba, 2019, Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Rukwa ambapo atazindua mradi wa maji na usafi wa mazingira wa Mji wa Sumbawanga, atazindua Msikiti wa Istiqaama Community of Tanzania uliopo Sumbawanga Mjini na atazungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanja wa Nelson Mandela Mjini Sumbawanga.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Sumbawanga

06 Oktoba, 2019

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa