• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Rais Magufuli agawa usafiri kwa maafisa tarafa Rukwa huku wakikisitizwa kutimiza majukumu ya serikali hasa kutoa elimu ya Corona.

imewekwa Tar: May 14th, 2020

Katika hatua za kuboresha utendaji kazi wa Maafisa Tarafa nchini Rais Wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli ametoa pikipiki 12 kwa Maafisa Tarafa mkoani Rukwa ili ziweze kuwasaidia kutekeleza majukumu yao ya kiserikali katika kata wanazozihudumia.

Pikipiki hizo zimetolewa ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa tarehe 04.06.2019 baada ya kufanya kikao kazi na Maafisa Tarafa wote nchini alipokutana nao Ikulu Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi pikipiki hizo Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alimshukuru Rais kwa kutimiza ahadi hiyo huku akiwasisitiza maafisa hao kuzitumia pikipiki hizo kwa malengo yaliyokusudiwa na Rais ikiwemo kusimamia mapato, miradi ya maendeleo iliyopo kwenye maeneo yao pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Alieleza kuwa katika ziara zake alizozifanya katika maeneo ya vijijini, alibaini kuwepo kwa mwamko mdogo wa wananchi juu ya ugonjwa hatari wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19) hivyo kuwataka maafisa hao kuhakikisha wanavitumia vyombo hivyo kufikisha elimu ya ugonjwa huo hatari.

“Ni Imani yangu kuwa tutavitumia vyombo hivi vya usafiri kuhakikisha kuwa tunawafikia wananchi wetu kwenye maeneo yao ili tuweze kuwahamasisha kujikinga na ugonjwa huu hatari ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka mara kwa mara na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima,” Alisema

Aidha, Alimtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa kuhakikisha anachukua hatua kali za kisheria na kiutumishi kwa Afisa Tarafa yeyote atakayetumia pikipiki hiyo kinyume na malengo ya serikali ikiwemo kutumia kama Bodaboda na kuongeza kuwa pikipiki hizo zina namba za serikali, hivyo, kuzitumia kinyume na malengo yake ni ukosefu wa maadili.

Kwa upande wake Katibu Tawala huyo wakati akieleza mgawanyo wa pikipiki hizo alisema kuwa Mkoa wa Rukwa una Tarafa 16 ambapo Tarafa 4 kati ya hizo zina pikipiki ambazo zimekaguliwa na ziko salama zinaendeelea kufanya kazi na hivyo kuwasisitiza maafisa hao kutekeleza majukumu yao kama yalivyoainishwa katika Waraka Namba 1 wa Maendeleo ya Utumishi wa Umma wa Mwaka 2007.

“Tarafa ambazo hazikuwa na usafiri kwa wilaya ya Kalambo ni Tarafa ya Matai, Kasanga, Mwimbi, Mwazye na Mambwenkoswe zilikuwa hazina usafiri. Kwa Wilaya ya Sumbawanga ni Tarafa ya Itwelele, Kipeta, Lwiche na Mtowisa  na Wilaya ya Nkasi ni Tarafa ya Chala, Kate na Namanyere na tarafa ambazo zilikuwa na pikipiki kwa Wilaya ya nkasi ni Wampembe na Kirando na Wilaya ya Sumbawanga ni Laela na Mpui,” Alisema.

Wakati akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Maafisa Tarafa wenzake, Afisa Tarafa ya Kasanga Andrew Ngindo baada ya kumshukuru Rais Magufuli, alimuomba Mkuu wa Mkoa kuona uwezekano wa kutengewa bajeti ya mafuta pamoja na matengezo kwa pikipiki hizo ili ziendelee kuwarahisishia utekelezaji wa majukumu yao.

“Kuwa na Pikipiki ni jambo moja lakini pikipiki ikiwa bila ya Mafuta bila ya uwezeshwaji wa kutosha ni kama tembo mweupe ndani ya nyumba, mimi niwaombe sana wakuu wa wilaya, sisi ndio wawakilishi wao katika maeneo yale ambayo wao wasipofika sisi tukifika maana yake Mkuu wa Wilaya amefika na tayari tumekuwa tumetekeleza makujumu yao, kwahiyo Wakuu wa wilaya watusaidie kupata bajeti hiyo,” Alisema.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli aliahidi kuwapa usafiri maafisa tarafa wote nchini wasio na usafiri na hivyo kutoa pikipiki 448 kote nchini kwaajili ya maafisa hao ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa