• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Rais Magufuli azindua uandikishaji orodha ya wapiga kura Serikali za Mitaa Nkasi

imewekwa Tar: October 8th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 08 Oktoba, 2019 amefungua barabara ya Sumbawanga – Kanazi, ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi, amefungua Kituo cha Afya Nkomolo na kuzindua uandikishaji katika orodha ya wapiga kura wa Mamlaka za Serikali za Mitaa (2019) ulioanza leo hapa nchini.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale amesema ujenzi wa barabara ya Sumbawanga – Kanazi yenye urefu wa kilometa 75 ambayo ni sehemu ya barabara ya Sumbawanga – Kanazi – Mpanda yenye urefu wa jumla ya kilometa 245, uliogharimu shilingi Bilioni 100.7 umekamilika mwaka 2017 na barabara hiyo imekabidhiwa mwaka 2018.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amesema Hospitali ya Wilaya ya Nkasi ambayo inajengwa kwa ghamara ya shilingi Bilioni 1 na Milioni 500 ni moja kati ya hospitali mpya 69 zenye hadhi ya Wilaya zinazojengwa hapa nchini na kwamba katika bajeti ya mwaka huu Serikali imetenga fedha za ujenzi wa Hospitali zingine 27 na kufanya jumla ya hospitali zenye hadi ya wilaya zilizojengwa katika Awamu ya tano kufikia 96.

“Mhe. Rais tunakushukuru na kukupongeza sana kwa kutoa kipaumbele katika ujenzi wa miundombinu ya kutolea huduma za afya, kwa miaka miwili tu unajenga Hospitali za Wilaya 96 wakati nchi yetu tangu ipate uhuru ilifanikiwa kujenga Hospitali za Wilaya 77 tu hadi mwaka 2015” amesema Mhe. Jafo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Namanyere, Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa.

Kituo cha Afya Nkomolo kilichojengwa kwa gharama ya shilingi Milioni 500 tayari kimeanza kutoa huduma na kimefunguliwa kwa niaba ya vituo vingine 10 vya Mkoa wa Rukwa ambavyo vimejengwa katika Wilaya zote za Mkoa huo.

Mhe. Rais Magufuli amezindua uandikishaji katika orodha ya wapiga kura wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao umeanza nchini kote leo tarehe 08 Oktoba, 2019 hadi tarehe 14 Oktoba, 2019 na amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kushiriki kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowafaa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 24 Novemba, 2019.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara Mjini Namanyere, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Nkasi na Mkoa mzima wa Rukwa kwa maendeleo makubwa ya kuimarishwa kwa miundombinu ya barabara, hospitali, vituo vya afya, umeme na huduma nyingine na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha zaidi maisha ya wananchi.

Mhe. Rais Magufuli ambaye akiwa njiani kutoka Sumbawanga kwenda Namanyere Wilayani Nkasi amesalimiana na wananchi wa Ntendo, Nkundi, Milundikwa, Kasu na Chala amewataka wataalamu wa Wizara ya Maji kubadilika na kubuni mbinu za kutatua matatizo ya maji yanayowakabili wananchi, ikiwemo kuvuna maji ya mvua katika mabonde yaliyopo katika maeneo mengi yenye tatizo la ukosefu wa maji.

Akiwa katika mkutano huo wa hadhara, Mhe. Rais Magufuli amesikiliza kilio cha Mama Mjane aitwaye Felista Mkombo ambaye aliibiwa ng’ombe 25 lakini Askari Polisi walimwachia mtuhumiwa na baadaye akafanikiwa kutoroka, ambapo ameagiza Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa Mathias Nyange na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Said Mtanda kumlipa Mama huyo shilingi Milioni 15 kama fidia kutokana na kutoshughulikia vizuri tatizo lake.

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa na namna viongozi wa Mkoa wa Rukwa wasivyoshughulikia kero za wananchi na mara baada ya kumaliza hotuba yake ameagiza viongozi hao wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Joachim Wangabo kubaki mkutanoni hapo ili wasikilize kero za wananchi wote waliokuwa wamebeba mabango na kumpatia taarifa.

“Tatizo la Mkoa huu viongozi hamshughulikii kero za wananchi, kila mahali wananchi wanalalamika na hata hapa kuna mabango mengi ya wananchi wenye kero mbalimbali, sasa nataka mbaki hapa muwasikilize na mnipe taarifa” ameagiza Mhe. Rais Magufuli.

Amempongeza Mbunge wa Nkasi Mhe. Ally Kessy kwa jinsi anavyoshughulikia kero za wananchi na kufuatilia miradi ya maendeleo na amemuahidi kuwa Serikali itachukua hatua kutatua kero hizo pamoja kuwachukulia hatua watumishi wa umma ambao wamekuwa wakishirikiana na wakandarasi kuiba fedha za miradi.

Kesho tarehe 09 Oktoba, 2019, Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli ataendelea na ziara yake ambapo atafungua barabara ya Kanazi – Kizi – Kibaoni.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Namanyere, Nkasi

08 Oktoba, 2019

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa