• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Akemea Ushirikina

imewekwa Tar: November 4th, 2022

SENDIGA: ‘NI AIBU RUKWA KUENDEKEZA IMANI ZA KISHIRIKINA’

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa Queen Sendiga akemea kikundi cha matapeli kilichoibuka mkoani humo maarufu kama rambaramba ambao wanasababisha taharuki kwenye jamii wakisaka washirikina.

Ametoa onyo hilo leo (Alhamisi, Novemba 03,2022) wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha King’ombe kata ya Kala wilaya ya Nkasi ambapo kwa siku za hivi karibuni matapeli hao wamekuwa wakichangisha fedha ili waondoshe ushirikina.

Sendiga ametoa agizo hilo kufuatia hivi karibuni kutokea kikundi cha watu wanaofanya utapeli kwa kupita kwenye makazi ya watu na kusaka wachawi hatua inayopelekea taharuki kwenye wilaya za Nkasi, Kalambo na Sumbawanga.

“Mnaharibu sifa nzuri ya mkoa wetu, watu wanakimbia nyumba zao kwa kuogopa rambaramba kufika kusaka wachawi. Kata hii inaongoza kwa kufanya vikao vya kusaka wachawi. ” alisema  Sendiga.

Katika mkutano huo, Sendiga ametoa agizo kwa Jeshi la Polisi kuendesha msako na kuchukua hatua za kuwafikisha mahakamani watu wanaoendeleza vitendo vya kusaka wachawi kwenye makazi ya watu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Peter Lijualikali amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa ataongoza kampeni maalum ya kuwasaka watu wanaofanya utapeli kwa kigezo cha kusaka wachawi kwenye makazi ya watu na kukusanya fedha kwa watu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amefanya ukaguzi wa vituo vya afya Kate na Kala ambavyo vimepokea kila kimoja shilingi Milioni Mia Tano (500,000,000) zilizotokana na tozo ambapo ameagiza Halmashauri kuhakikisha vituo hivyo vinakamilika kabla ya mwaka 2022 kuisha.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa