• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

imewekwa Tar: January 29th, 2026


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere amefanya ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo Januari 29, 2026.

Ziara hiyo ni sehemu ya ziara zake za ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika sekta mbalimbali mkoani Rukwa.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mheshimiwa Makongoro amesisitiza umuhimu wa taasisi za umma kuwa na hati miliki za maeneo yanakotekelezwa miradi ya maendeleo.


Amebainisha kuwa umiliki wa ardhi ni msingi wa kulinda rasilimali za umma na kuwezesha upanuzi wa huduma kulingana na mahitaji ya sasa na ya baadaye.


Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Makongoro ameelekeza taasisi hizo kuongeza ukubwa wa maeneo yao pale inapohitajika ili kuepuka changamoto za uhaba wa ardhi katika siku zijazo.

Vilevile, Mheshimiwa Makongoro amewaagiza viongozi wa shule na vituo vya kutolea huduma za afya kupanda miti ya matunda katika maeneo yao.


Amesema hatua hiyo itachangia uhifadhi wa mazingira pamoja na kuboresha lishe kwa wanafunzi, wagonjwa na jamii inayozunguka taasisi hizo.


Aidha, Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo uzingatie viwango vya ubora, thamani ya fedha na ukamilishaji kwa wakati.

Amesema lengo ni kuhakikisha wananchi wananufaika na huduma zinazotolewa na Serikali kwa ufanisi na kwa wakati stahiki.


Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Makongoro ametembelea na kukagua ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Ikozi.


Pia ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Shule ya Msingi Mzindakaya na Zahanati ya Mshani.

Kadhalika, amekagua miundombinu ya nyumba za walimu katika Shule ya Wasichana Rukwa na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Zahanati ya Kavifuti.


Miradi hiyo inalenga kuboresha utoaji wa huduma za elimu na afya kwa wananchi wa Wilaya ya Sumbawanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa