• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa aagiza kufuata utaratibu uingizwaji wa mahindi kutoka nchi za jirani.

imewekwa Tar: October 24th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen ameziagiza Halmashauri zote Mkoani kwake kuhakikisha wanakuwa na magulio rasmi ya kuuzia mahindi ili wakulima na wafanyabiashara waweze kufuata utaratibu.

Amesema kuwa kwa kufanya hivyo kutakuwa na usimamizi thabiti na taratibu za uingizwaji wa bidhaa kutoka katika nchi za jirani utafuatwa pamoja na mamlaka husika kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa sheria zilizopo ikiwa ni pamoja na halmashauri kupata mapato na nchi kwa ujumla.

Kauli hiyo ameitoa baada ya kufanya ziara ya ghafla katika Kijiji cha Safu, kilichopo mpakani mwa Tanzania na Zambia na kujionea malori yenye shehena za mahindi yakiingizwa kiholela kutoka katika nchi ya Zambia bila ya kuwepo kwa mamlaka husika zinazosimamia uingizwaji wa bidhaa kutoka katika nchi za jirani.

“Ni mategemeo yangu kuwa wakurugenzi wataanzisha vituo ili wakulima waweze kupeleka mazao yao hapo na kuweza kuyauza na ndipo nao halmashauri waweze kukusanya ushuru unaotakiwa, lakini hizi biashara zinazofanywa kupitia njia za panya, nasema si kitu cha kuachiwa, hivyo basi nisingependa kuona malori yanaruhusiwa kwenda maeneo ambayo siyo mipaka rasmi kuchukua mizigo na kuingiza nchini,” Amesema.

Na kuongeza kuwa hakuna tatizo kufanya biashara na nchi za jirani isipokuwa biashara hizo zifanywe kihalali kwa kufuata sheria zilizowekwa.

Halikadhalika Mh. Zelote Alisema kuwa Mkoa wa Rukwa una mahindi ya kutosha na wafanyabiashara wa mikoa mingine wafike kununua na sio kuvuka mipaka kwa njia za kupanya kufanya biashara hiyo.

Kwa upande wao wafanyabiashara waliohojiwa na Mh. Zelote katika ziara yake hiyo walidai kuwa mahindi yanayotoka Zambia bei yake ni nafuu zaidi kuliko ya Tanzania lakini pia wakulima wa Tanzania huficha mahindi yao wakisubiri kupanda kwa bei jambo ambalo ni hasara kwa wafanyabiashara wanaotoka nje ya Mkoa wa Rukwa.

“Wakulima wa Mkoa wa Rukwa huficha mazao yao wakisubiri kupanda kwa bei, sasa kama mimi mfanyabiashar natokea Mwanza nakuja kwa mahesabu ya kuchukua mzigo na kuondoka, nikisema nimsubiri huyu mkulima aliyeficha mazao yake hadi yaapande mimi nakula hasara,” Amiri Giti mfanyabiashara kutoka Mwanza alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa