• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa asikitishwa na utendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga

imewekwa Tar: July 23rd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna mstaafu Zelote Stephe amesikitishwa na kitendo cha halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kuwa na hoja za kujibu zipatazo 60 ambazo zimesababisha halmashauri hiyo kupata hati ya mashaka wakati halmashauri hiyo imeajiri watumishi wenye uwezo wa kuepusha jambo hilo lisijitokeze.

Akizungumza katika kikao cha baraza la dharula la madiwani Jana Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa anasikitishwa sana na kitendo hicho kwani wataalamu hao wameajiriwa huku serikali ikiwa inamatumaini kuwa ni watu wenye uwezo sasa zinapotokea hoja hizo yeye binafsi zinamsikitisha sana.

Alisema kuwa halmashauri hiyo haipaswi kuwa na huruma na watu wote waliosababisha hoja hizo kwani wanaoumia ni wananchi kutokana na baadhi ya watendaji kusababisha hali hiyo ambayo inapelekea halmashauri kupata hati ya mashaka na hata chafu na yeye akiwa ni Mkuu wa mkoa hatakubaliana na hilo.

"Binafsi nachukizwa sana na hali hii, siipendi hata kidogo kwani inaumiza na kuonekana hatuna watendaji wenyeuwezo, abadani sitakubali hali hii katika mkoa wangu labda uwe mkoa mwingine," Alisema.

Aliongeza kuwa madiwani wanapaswa Kutambua kuwa wao ndio taa ya halmashauri, kwani wakilegalega na halmashauri ikiendelea kupata hati ya mashaka wajue watakwenda kujibu wenyewe kwa wananchi ambao wamewatuma kuwawakilisha ili kuleta maendeleo katika halmashauri. 

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Mh.Kalolo Ntila alisema kuwa hoja hizo hazikutokana na baraza lililopo hivi sasa, na hata Mkurugenzi aliyopo hivi sasa na kuahidi kuwa wale wote waliosabaisha hoja hizo lazima watafutwe popote waliopo na kuchukuliwa hatua.

" hatutawaacha watu hawa bali tunazipitia hoja moja baada ya nyingine na kuzitolea majibu,lakini zile ambazo kitakuwa na matatizo ni lazima waliopo sababu sha wasakwe popote walipo na hatua dhidi yao zichukuliwe" alisema

Awali akizungumza katika baraza hilo la madiwani Mkaguzi mkazi na mdhibiti wa hesabu za serikali John Nalwambwa alisema kuwa ofisi yake ilibaini kuwepo kwa hoja 60 zenye utata ambapo hoja 25 kati ya hizo ndizo zilizopelekea kupata hati ya mashaka.

Alisema kuwa kuna fedha zaidi ya shilingi milioni 40 ambazo hazieleweki vizuri matumizi yake na baadhi ya vitabu vya makusavyo vikiwa vimepotea na hivyo nilazima ifahamike hatma ya suala hilo.

Alisema kuwa ofisi yake imefanya kazi kwa weledi mkubwa bila kuonea mtu na ndiyo imebaini hayo hivyo basi ni jukumu la halmashauri kuona ni jinsi gani itajibu hoja hizo ili zisijirudie tena.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa