• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa asisitiza mambo matatu kwa madiwani kikao cha PS3

imewekwa Tar: May 16th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kmaishna Mstaafu Zelote Stephen amewasisitiza madiwani kufuatilia miradi, kusimamia mapato na utawala bora ili Halmashauri za mkoa wa Rukwa ziweze kuendelea na kufikisha huduma bora kwa wananchi.

Aliyasisitiza hayo alipokuwa akifungua mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi pamoja na Manispaa ya Sumbawanga zote za Mkoa wa Rukwa siku ya tarehe 15 Mei, 2017. Mafunzo yanayoendeshwa na mradi wa PS3  unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la watu wa Marekani USAID.

Katika kuyafafanua kila jambo Mh. Zelote alianza kwa kuwasisitiza waheshimiwa Madiwani Kufuatilia na kufanya tathmini ya miradi yote inayotekelezwa na Halmashauri zetu.

Mh. Zelote aliwakumbusha fedha zinazotoka Serikali kuu na kupelekwa Serikali za Mitaa na kutumika katika utekelezaji wa miradi ya sekta mbalimbali ikiwemo, Elimu, Afya, Maji, Barabara namengineyo. Hivyo aliwasisitiza kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ubora unaotarajiwa.

“Nimekuwa nikifanya ziara nyingi sana katika kata mbalimbali zenye miradi hii, na nikifika huko naona namna miradi hiyo inavyotekelezwa chini ya viwango mpaka huwa najiuliza hivi kuna diwani kweli kwenye kata hii, mbona miradi hii ambayo ni faida kwa wananchi inakuwa haieleweki?” Mh. Zelote alieleza.

Kwa upande wa kusimamia mapato Mh. Zelote aliwatahadharisha madiwani hao kuwa kama Halmashauri haitakusanya mapato ya kutosha maana yake Halmashauri haitakuwepo jambo litakalopelekea wananchi kukosa huduma muhimu na kucheleweshewa maendeleo.

“Watumishi wote katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wafanye kazi kwa juhudi na maarifa na pia waepuke kufanya kazi kwa mazoea ili kuimarisha ukusanyaji wa mapato, na Wakurugenzi wa halmashauri zote wasimamie vizuri ukusanyaji wa mapato,” Mh. Zelote alisisitiza.

Katika kuhakikisha madiwani wanaelewa maana ya utawala bora katika kupeleka maendeleo kwa wananchi Mh. Zelote alisisitiza kuwa maendeleo hayana vyama, dini, ukabila na kwamba wadau wote wa maendelo wanapaswa kushirikiana kwa pamoja ili wananchi wote wapate maendeleo kwa usawa.

Mkuu wa Mkoa alisema, “Ili wananchi wawe ni sehemu ya maendeleo ya miradi inayopelekwa katika maeneo yao basi waheshimiwa madiwani ndio madaraja ya kupeleka maendeleo hayo, hivyo wao wanatakiwa kuwa kitu kimoja na kuachana na itikadi za kisiasa ili kuwafikishia wananchi maendeleo.”

Katika kukazia yale aliyoyazungumza Mh. Zelote aliwaomba madiwani hao kuyatumia vizuri mafunzo hayo yaliyotolewa na mradi wa Public Sector Strengthening System (PS3) na kuwashukuru watu wa Marekani ambao kwa kupitia shirika lao la Maendeleo USAID wameweza kufadhili mafunzo hayo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa