• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Sendiga Akutana na Wazee

imewekwa Tar: September 12th, 2022

RC SENDIGA AKUTANA NA WAZEE WA RUKWA, AOMBA USHIRIKIANO

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amewaomba wazee na viongozi wa madhehebu ya dini kuunga mkono jitihada za Serikali kusukuma agenda za maendeleo ili mkoa upige hatua za kiuchumi.

Sendiga amewasihi wazee hao kuliombea taifa na viongozi wake ili mipango inayowekwa izingatie maslahi mapana ya taifa na kujibu changamoto za maendeleo ya Rukwa hatua itakayowezesha ustawi wa jamii.

Mkuu huyo wa Mkoa ameyasema hayo leo (12.09.2022) mjini Sumbawanga wakati wa kikao na wazee pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini toka katika wilaya zote tatu za mkoa wa Rukwa akiwa na lengo la kujitambulisha kwao na kuwaelezea mipango inayotekelezwa na Serikali.

“Nawaomba msaidie kuombea nchi yetu, tumwombee pia Rais wetu Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuiongoza nchi yetu vema katika kujiletea maendeleo kwani malengo yake ni mizuri”, alisema Sendiga.

Katika kikao hicho Sendiga aliwaeleza wazee kuwa wanalo jukumu la kusaidia na kushauri viongozi na watendaji wa Serikali ili shughuli za maendeleo za mkoa wa Rukwa ziwe kwa ubora hatua itakayoondoa changamoto kwa wananchi.

Nao wazee kwa nyakati tofauti akiwemo Honarama Mwimanza mkoani wa Sumbawanga alimkaribisha mkuu huyo kwenye mkoa wa Rukwa na kumsihi afuate nyendo za Rais Samia Suluhu Hassan katika kusimamia shughuli za maendeleo ya watu.

Kuhusu utekelezaji wa miradi , Meda Chipamba Mwenyekiti wa Wazee Kata ya Mazwi aliomba uongozi wa mkoa uwe na usimamizi wa karibu wa watendaji na wakandarasi wa miradi ili ikamilike kwani wananchi wengi wanakerwa na miradi mingi kutoisha.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Sendiga ametoa miezi miwili kwa Katibu Tawala Mkoa huo Rashid Mchatta kukaa pamoja na wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanamaliza tatizo la uwepo wa maboma ya shule yasiyokamilika na kupelekea watoto kukaa chini.

Sendiga ameyasema hayo leo wakati akizindua miongozo ya kuboresha elimu na kuongeza “Natamani kuona sekta ya elimu ikipiga hatua, usisikie raha kuona mkoa wetu uko nyuma kielimu” alisema Sendiga.

Mwisho.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa