• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Sendiga Akutana na Wazee

imewekwa Tar: September 12th, 2022

RC SENDIGA AKUTANA NA WAZEE WA RUKWA, AOMBA USHIRIKIANO

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amewaomba wazee na viongozi wa madhehebu ya dini kuunga mkono jitihada za Serikali kusukuma agenda za maendeleo ili mkoa upige hatua za kiuchumi.

Sendiga amewasihi wazee hao kuliombea taifa na viongozi wake ili mipango inayowekwa izingatie maslahi mapana ya taifa na kujibu changamoto za maendeleo ya Rukwa hatua itakayowezesha ustawi wa jamii.

Mkuu huyo wa Mkoa ameyasema hayo leo (12.09.2022) mjini Sumbawanga wakati wa kikao na wazee pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini toka katika wilaya zote tatu za mkoa wa Rukwa akiwa na lengo la kujitambulisha kwao na kuwaelezea mipango inayotekelezwa na Serikali.

“Nawaomba msaidie kuombea nchi yetu, tumwombee pia Rais wetu Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuiongoza nchi yetu vema katika kujiletea maendeleo kwani malengo yake ni mizuri”, alisema Sendiga.

Katika kikao hicho Sendiga aliwaeleza wazee kuwa wanalo jukumu la kusaidia na kushauri viongozi na watendaji wa Serikali ili shughuli za maendeleo za mkoa wa Rukwa ziwe kwa ubora hatua itakayoondoa changamoto kwa wananchi.

Nao wazee kwa nyakati tofauti akiwemo Honarama Mwimanza mkoani wa Sumbawanga alimkaribisha mkuu huyo kwenye mkoa wa Rukwa na kumsihi afuate nyendo za Rais Samia Suluhu Hassan katika kusimamia shughuli za maendeleo ya watu.

Kuhusu utekelezaji wa miradi , Meda Chipamba Mwenyekiti wa Wazee Kata ya Mazwi aliomba uongozi wa mkoa uwe na usimamizi wa karibu wa watendaji na wakandarasi wa miradi ili ikamilike kwani wananchi wengi wanakerwa na miradi mingi kutoisha.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Sendiga ametoa miezi miwili kwa Katibu Tawala Mkoa huo Rashid Mchatta kukaa pamoja na wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanamaliza tatizo la uwepo wa maboma ya shule yasiyokamilika na kupelekea watoto kukaa chini.

Sendiga ameyasema hayo leo wakati akizindua miongozo ya kuboresha elimu na kuongeza “Natamani kuona sekta ya elimu ikipiga hatua, usisikie raha kuona mkoa wetu uko nyuma kielimu” alisema Sendiga.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa