• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Sendiga: Tutafanya Mapinduzi ya Kilimo Rukwa

imewekwa Tar: August 11th, 2022

RC SENDIGA:  TUTAFANYA MAPINDUZI YA KILIMO RUKWA

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amesema anatarajia kuona mkoa wa Rukwa ukifanya mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo kiwe cha kibiashara na kukuza uchumi wa wananchi.

Ili kufanikisha hilo amewataka wataalam wa kilimo katika halmashauri zote nne za Rukwa kuja na mikakati ya kufanya kilimo kichangie zaidi katika kukuza pato la wananchi na kuongeza uhakika wa chakula.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema hayo jana mjini Sumbawanga (10 Agosti, 2022) wakati wa hafla rasmi ya makabidhiano ya ofisi toka kwa mtangulizi wake Joseph Mkirikiti kufuatia Rais Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.

“Natamani kuiona Rukwa ikifanya mapinduzi makubwa katika kilimo. Maafisa kilimo na ugani jitahidini kuwa na mipango mizuri ili kilimo chetu kiwe cha kibiashara na kuhusisha vijana wengi “alisema Sendiga.

Sendiga aliongeza kusema mkoa lazima uwe na mkakati wa kufanya vijana wengi kurudi vijijini ili kufanya kazi za kilimo hatua itakayowapatia uhakika wa ajira hivyo kutimiza lengo la Rais Samia kutaka kuona kilimo kuzalisha ajira nyingi nchini.

Katika hatua nyingine Sendiga amewaeleza wananchi kuwa atapenda kuona mkoa wa Rukwa ukipiga hatua kubwa katika sekta ya elimu ili watoto wengi zaidi wafaulu mitihani na taaluma kukua zaidi.

Kuhusu usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma, Sendiga ametoa rai kwa halmashauri za Rukwa kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato ili fedha nyingi zaidi zitumike kutekeleza miradi ya maendeleo.

“Natamani wataalam wa halmashauri waje na mipango madhubuti ya ili tuwe na miradi inayokamilika kwa wakati .Sipendi kuona maboma yasiyokamilika kwenye halmashauri zetu” alisisitiza Sendiga.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa anayemaliza muda wake Joseph Mkirikiti alitumia nafasi hiyo kuwaaga wana Rukwa ambapo amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumwamini kipindi alichoongoza mkoa huo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Rainer Lukala akizungumza kwenye hafla hiyo alimpongeza Mkuu wa Mkoa mpya ambapo alimtaka kushirikiana na chama hicho kutekeleza Ilani ya Uchaguzi.

“Tunaamini kazi unayokuja kufanya Mkuu wetu mpya wa Mkoa (Sendiga) ni usimamizi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ili wananchi wa Rukwa wapate maendeleo. Tuko tayari kushirikiana nawe” alisema Lukala.

Lukala aliongeza kusema wanampongeza Mkuu wa Mkoa aliyepita Joseph Mkirikiti kwa ushirikiano wake na chama na kuwa wamepokea mabadiliko yaliyofanywa na Rais vema.

Mkuu wa Mkoa Queen Sendiga anakuwa mkuu wa mkoa wa Rukwa wa 17 tangu ulipoanzishwa mwaka 1974.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa