• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aendelea kuelimisha wanarukwa juu ya ugonjwa wa Corona

imewekwa Tar: May 31st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo ameendelea kuwatahadharisha wananchi wa mkoa huo juu ya uwepo wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid – 19) na kuwataka kuendelea kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kufuata maelekezo yote ya wataalamu wa afya.

Aidha, amesisitiza kuendelea kujifukiza kwa kutumia majani yaliyoelekezwa na wataalamu, majani ambayo yanapatikana kwa wingi sana katika mkoa wa Rukwa na kuwaasa kutoona aibu kwani njia hizo zimekubaliwa na kiutambuliwa na taasisi za afya nchini pamoja na kurtumika na viongozi mbali mbali wa ngazi za juu nchini.

“Watu wanaambiana kwamba ugonjwa umeisha, haujaisha, ugonjwa wa Covid – 19 bado upo, na sisi mkoa wa Rukwa tumepata wagonjwa pia, wengine wamepona wengine bado, kwahiyo chukueni tahadhari, ugonjwa bado upo na Mheshimiwa Rais wetu kipenzi cha watanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amekwisha tahadharisha pia kwamba ugonjwa huu upo, ila tumshukuru Mwenyezi mungu sana kwasababu ukali wa ugonjwa huu sio kama ilivyotokea kule Marekani, Hispania, Italy na kwingineko, tuna unafuu mkubwa sana kwahiyo tumshukuru Mwenyezi mungu kwa jambo hili,” Alisema.

Halikadhalika aliwataka wananchi hao kuendelea kutumia nyumba za ibada kufanya maombi na kuwasihi kuendelea vyombo vya kunawia katika nyumba hizo za ibada pamoja na kuvaa barakoa kwenye mikusanyiko hiyo huku akieleza umuhimu wa barakoa kuwa ni kubaki na vimelea vyako wakati wa kukohoa ama kupiga chafya ili visisambae kwa wengine na kuwaletea madhara.

“Umuhimu wake ni kwamba mimi ninapoongea kama hivi, tunapopeana mita mbili tatu, tunapoongea mate yanatoka, yanapotoka yaishie kwenye barakoa, ndio maana tunazivaa, hatuvai kama vile mapambo na kuwa tumeelekezwa tu tuvae, hapana, lakini pia unazuia pale ambapo mwenzako anaongea yale mate yake yasikufikie wewe, ni lazima tutumie barakoa ili kuhakikisha kwamba maambuki haya yasikufikie wewe ama yasimfikie mwenzako kama wewe unayo bila ya kufahamu,” Alitahadharisha.

Pia alieleza kuwa endapo mtu atapatwa na dalili za ugonjwa huo ambazo ni homa kali, vidonda vya kooni, mwili kuchoka, na kukohoa mara kwa mara akimbilie katika kituo cha kutolea huduma za afya ili ajue hali yake na kuchukua hatua stahiki.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa