• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aishauri Wizara ya Kilimo kujenga vihenge eneo la viwanda la Kanondo.

imewekwa Tar: January 16th, 2019

Katika hali ya kuupendezesha mji wa Sumbawanga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameishauri wizara ya kilimo nchini kuona namna ya kuhamisha mradi wa ujenzi wa vihenge kutoka katikati ya mji wa Sumbawanga na kuhamishia katika eneo maalum lililotengwa na Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kwaajili ya ujenzi wa maghala na viwanda ili kuutanua mji na kujenga vihenge hivyo kwa nafasi.

Amesema kuwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)tayari wamekwishanunua eneo la ekari 24.6 lenye thamani ya shilingi 298,938,000 lililopo katika eneo maalum lililotengwa kwaajili ya viwanda vidogo, maghala na hotel lililopo Kijiji cha Kanondo, Kata ya Ntendo, Manispaa ya Sumbawanga ambapo mpaka sasa viwanja vilivyouzwa katika eneo hilo ni asilimia 35.

“Sisi tungependa kama mkoa wa Rukwa eneo hili liwekezwe, kwasababu tuna uchumi wa kati wa viwanda, lakini sasa naona bado tunapenda maeneo yet utu, sasa huku nani atakuja aendeleze? Kwakweli huu mradi uje kujengwa huku ntashauriana na wizara ya kilimo..Mh. Waziri..tuone namna ya kuleta huku, kwasababu hapo mnapotaka kujenga ni eneo dogo” Alisema.

Ameyasema hayo alipotembelea eneo hilo maaluma la uwekezaji wa maghala lililililonunuliwa na NFRA miaka miwili iliyopita huku likiwa limeachwa wazi bila ya matumizi yoyote.

Kwa upande wake Kaimu meneja wa NFRA Mkoa wa Rukwa James Marwa alisema kuwa mradi wa vihenge ulianza kabla ya kununuliwa kwa eneo hilo, hivyo ili kuhamisha mradi huo lazima eneo hilo jipya lipimwe upya.

Nae Afisa Mipango miji wa Manispaa ya Sumbawanga Thadeo Maganga amesema kuwa hatachoka kuendelea kuwahamasisha wadau mbalimbali kufika katika eneo hilo ili kuona umuhimu wake na kuweza kuwekeza kwa maslahi ya Manispaa, Mkoa nan chi kwa ujumla.

Ujenzi huo wa Maghala na Vihenge vya kisasa (Silos) utajengwa katika maeneo nane ya kanda saba za wakala ambapo ujenzi huo utaongeza uwezo wa kuhifadhi mahindi kutoka Tani 251,000 za sasa hadi Tani 700,000 ifikapo mwaka 2025.

Mradi huo wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi umeanza kujengwa katika Manispaa ya Songea (Ruvuma), Dodoma, Mpanda (Katavi), Makambako (Njombe), Mbozi (Songwe), Sumbawanga (Rukwa), Shinyanga Mjini (Shinyanga), na Babati (Manyara) ambapo Serikali ya Tanzania na Serikali ya Poland zilisaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu Septemba 2015 wa Dola milioni 55 sawa na sh. bilioni 124, kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo, ambao utaongeza uwezo wa hifadhi ya chakula.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa