• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aitaka idara ya Kilimo kujipanga kitakwimu baada ya upungufu wa mbolea kushtusha.

imewekwa Tar: January 18th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Katibu tawala wa Mkoa Bernard Makali kuitisha kikao maalum cha wataalamu wa kilimo kutoka katika Halmashauri zote Mkoani humo ili kubaini mahitaji sahihi ya mbolea kwa manufaa ya sasa nay a baadaye.

Amesema kuwa wataalamu wanaelewa kiasi cha mbolea inayohitajika kulingana na hekta za zilizopo katika Mkoa kwa kukokotoa hesabu na kupata jibu sahihi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo ili takwimu hizo zifanane.

“Katibu Tawala itisha kikao cha wataalamu wote wa kilimo kutoka katika Halmashauri zote, mkae mtafakari na kuja na takwimu sahihi, takwimu zikitupotosha tunapotea wote hata serikali inapotea kwasababu tunaweza kuagiza kiasi kikubwa mno na kupoteza pesa nyingi kumbe mahitaji ni kidogo, na ndio maana kunakuwa na sense hata za watu ili watu wapange mambo yao vizuri, kwenye Kilimo kuna lega leg asana,” Ameeleza.

Amesema kuwa walio wengi wanafanya kazi kwa ubabaishaji ambao unaonekana kwenye takwimu ambapo hapo awali ilionekana kuwepo na uhitaji wa tani 97,000 tofauti na takwimu zilizopo sasa zinaonyesha kuwepo kwa uhitaji wa tani 27,000 ambapo kati ya hizo tani 11,000 tayari zimepatikana ikiwa tani 5,000 za UREA na tani 6,000 za DAP jambo mabalo haliendani na uhalisia maana uhitaji wa mbolea kwa sasa sio mkubwa baada ya tani hizo kufika kulinganisha na tani tunazozisubiri.

Katika kuhakikisha idara hiyo inafanya kazi yake kwa ufanisi Mh. Wangabo amesema kuwa aliyekuwa akikaimu ukuu wa Idara hiyo katika ofisi yake amewekwa pembeni na kumpisha kaimu mwingine kwa malengo ya kuiboresha idara hiyo.

Amesema kuwa ikiwa ni miongoni mwa Mkoa unaotegemewa kwa uzalishaji wa chakula nchini haipendezi kwa idara hiyo kutokuwa na mpango sahihi wa maandalizi ya kilimo tangu kumalizika kwa msimu wa kilimo wa 2016/2017 hadi kuingia msimu wa kilimo wa 2017/2018 na kuiagiza idara hiyo kuwa karibu na waagizaji wakubwa wa mbolea kila ukikaribia msimu wa matayarisho ya mashamba kwa wakulima ili kujua kiasi cha mbolea kinachohitajika.

Ameyasema hayo katika kikao cha majumuisho ya ziara yake fupi ya kutembelea maghala ya wafanyabiashara wakubwa wa mbolea ya mjini sumbawanga ili kujionea changamoto na mafanikio yaliyofikiwa baada ya juhudi za serikali kuhakikisha kuwa Mkoa wa Rukwa unapata mbolea ya kutosha ili wakulima waweze kufikisha lengo la uzalishaji wa chakula katika Mkoa.

Kwa msimu wa 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulilima Hekta zipatazo 556,975.9 na kuvuna tani 1,109,055.6 za mazao ya chakula kati ya hizo mahindi yalikuwa tani 710,602. Kwa msimu huu wa Kilimo wa 2017/18 Mkoa umelenga kulima jumla ya eneo la Hekta 554,310.6 na kuvuna tani 1,669,746.2 za mazao ya chakula.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa