• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aonya kuhusu mimba mashuleni na Saratani ya mlango wa Kizazi

imewekwa Tar: April 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatahatharisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuwa makini na kushiriki katika tendo la ndoa katika umri mdogo kwani kufanya hivyo wanajiweka katika hatari ya kupata saratani ya mlango wa kizazi.

Amesema kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia kupata saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na kushiriki katika tendo la ndoa na wapenzi wengi, kuzaa watoto wengi, ndoa za mitala pamoja na uvutaji wa sigara.

“Tangu mwaka 2015 hadi 2017 kumekuwa na mimba 325 huku shule za msingi kukiwa na mimba zaidi ya 20, huu ni ushahidi kuwa wanafunzi mnashiriki katika vitendo hivi katika umri mdogo, tukijua wazi kuwa mwananfunzi wa shule ya msingi anamaliza shule akiwa na umri wa miaka 13 au 14 na wengi katika shule za sekondari, hili tendo linachangia upatikanaji wa saratani,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Mazwi ikishirikisha wanafunzi kutoka katika shule mbalimbali za msingi na sekondari zilizopo katika manispaa ya Sumbawanga.

Kwa upande wake mwakili wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Boniface Mokelemo ameusifu Mkoa wa Rukwa kwa kufanya vizuri katika mazoezi ya chanjo nyingine zinazoendelea nchini hivyo kuwa na Imani kuwa chanjo hii itafanya vizuri zaidi na kuwasihi wananchi kuhimizana kupata chanjo hiyo.

Katika kuliweka sawa hilo mganga mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu ameongeza kuwa mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa ilifanya vizuri kwa kuwafikia watoto wengi na kina mama wengi kupata chanjo kama surau, polio, pneumonia, na homa ya uti wa mgongo hali iliyopelekea kupungua kwa magonjwa mengi kwa watoto chini ya umri wa mwaka mmoja.

Kwa upande wao wanafunzi waliopata chanjo hiyo wamewaasa wanafunzi wenzao kutoogopa kushiriki kupata chanjo hiyo kwani itawasaidia kuwakinga na ugonjwa huo hatari wa saratani ya mlango wa kizazi na kuiomba serikali iweze kuwafikia wasichana wengi ili kuokoa maisha yao.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa