• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo apongeza mshikamano na kasi ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Nkasi

imewekwa Tar: April 19th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amepongeza mshikamano uliopo katika uongozi wa wilaya ya Nkasi unaongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Mh. Said Mtanda baada ya kuona namna uongozi huo ulivyojipanga katika kuhakikisha maelekezo na maagizo ya serikali yanatekelezwa kwa wakati hasa maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Nkasi.

Amesema kuwa mshikamano huo ni tunu kwa wanarukwa katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo na hasa linapokuja suala la utekelezaji wa upatikanaji wa huduma ambazo zinawagusa moja kwa moja wananchi waliokuwa wakisubiri huduma hizo kwa muda mrefu.

“Nimeona kwamba mmejipanga kwa kuleta vifaa, na kama hakuna vifaa ujenzi utasuasua, kuna mawe naona yanakwenda kwasababu yanahitajika kwa kasi kubwa, basi hilo eneo liwekewe nguvu kubwa sana, ndio eneo lenye hitaji kubwa kwa sasa na kama hakuna mawe tutashindwa kusogea hatua ya kuweka matofali hadi kufikia hatu ile ya linta,” alisema

Aliongeza kuwa hivi sasa mvua hakuna, hivyo ni wakati muafaka wa kuhakikisha vifaa vyote vinavyohitajika kwaajili ya ujenzi vinakuwa katika eneo hilo la ujenzi ili kila hatua ya ujenzi isikumbane na kikwazo cha kukosa vifaa na kutoa sababu ya mvua kuharibu barabara na hivyo vifaa kushindwa kufika.

Halikadhalika ametoa pongezi kwa namna vibarua wa ujenzi huo wanavyolipwa kwa wakati na kufanya kazi wakiwa wameridhika na malipo wanayopewa jambo linaloashiria kuwa ujenzi huo unakwenda bila ya dosari zozote na kuagiza kuwa hadi kufikia tarehe 10 Mei, 2019 majengo yote saba ya hospitali hiyo yawe yamefikia usawa wa linta ili kwenda na kasi ya utoaji huduma kwa jamii.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipokwenda kuona maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya wilaya inayojengwa katika makao makuu ya wilaya ya Nkasi mjini Namanyere ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa juu ya kuwataka Wakuu wa Mikoa kusimamia kwa karibu ujenzi wa hospitali hizo na hatimae kumalizika kwa wakati.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda alisema kuwa ili kuhakikisha vibarua na wagonga kokoto wanalipwa na mafundi walioingia nao mkataba, wameweka utaratibu wa mafundi hao kuwalipa mbele yake, zoezi linalofanyika katika ukumbi wa ofisi yake ya wilaya na wakati huo huo wakitumia fursa hiyo kuwapatia wagonga kokoto hao vitambulisho vya ujasiliamali.

Imeelezwa kuwa ili majengo saba ya hospitali hiyo yakamilike yanahitajika matofali 78,000 huku hadi tarehe 18 Aprili,2019 matofali 58,000 tayari yameshafyatuliwa ili kuendelea na ujenzi huo.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa