• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza kasi katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga.

imewekwa Tar: April 24th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo amemtaka Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kusimamia kwa karibu,  umakini na kuongeza kasi ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya sumbawanga baada ya kuona kusuasua kwa ujenzi huo tangu kuanza kwake tarehe 19 Januari, 2019 ambapo wananchi walijitokeza kuchimba misingi ya majengo saba ya hospitali hiyo.

Amesema kuwa muda mwingi umepita tangu kuanza kwa ujenzi huo na hadi sasa ilistahili uwe umefikia hatua ya lenta na matokeo yake bado ipo kwenye hatua ya jamvi pamoja na changamoto zilizokuwepo na kuongeza kuwa hali hiyo inawakatisha tamaa wananchi kwa kuona jengo halipandi tangu kuanza kushiriki kwao kwenye ujenzi huu na kutahadharisha kuwa kwa sasa hakuna sababu ya kusuasua katika ujenzi huo.

“Kuna haja kwa halmashauri kusimamia ujenzi huu kwa karibu kuanzia sasa hivi kasi iongezeke mara mbili hata tatu kwa ile iliyokuwepo kwasababu kuapanga matofali kwenda juu hata siku mbili ytatu unafika kwenye lenta lakini kutoka kule kwenye msingi kunahitaji uangalifu na kupanga vizuri zaidi, kwahiyo Mkurugenzi narudia tena simamia vizuri ujenzi wa hapa na kwa ukaribu zaidi,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipotembelea eneo la ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga inayojengwa katika Kijiji cha Mtowisa, Kata ya Mtowisa, bonde la ziwa Rukwa na kuwataka mafunzi wote waliokabidhiwa kujenga majengo saba ya hospitali hiyo kuhakikisha wanafikia ngazi ya lenta ifikapo tarehe 10 Mei, 2019 na kuongeza kuwa asiyefikia hatua hiyo atawajibishwa.

Wakati akisoma taarifa ya ujenzi wa hospitali hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Fani Musa aliwashukuru wananchi kwa kujitolea kwao kwa kazi za songambele zilizookoa shilingi 18,600,200 ikijumuisha kazi za kuchimba misingi ya majengo na mtaro wa kupeleka maji eneo la ujenzi, kusogeza tofali na ujazaji wa kifusi kwenye majengo hayo.

“Kwa ujumla kazi inaenda vizuri kwa mujibu wa ratiba ya kazi na tunatarajia kuikamilisha kwa wakati kama ilivyoelekezwa. Halmashauri inahitaji ushirikiano wa viongozi wote uendelee kama sasa ili kufikia mafanikio na kukamilisha ujenzi huu wa hospitali kwa muda uliopangwa,”Alisema

Ili kukamilisha ujenzi wa majengo saba ya hospitali hiyo ambayo ni majengo ya Utawala, Kufulia, Dawa, OPD, Maabara, Mionzi na Wazazi ni matofali 84,000 yanahitaji ambapo hadi sasa matofali 70,666 yameshafyatuliwa huku shilingi milioni 496 zikiwa zimeshatumika.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa