• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza kuyaongeza thamani mazao

imewekwa Tar: March 25th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatakaka wakulima wa Kijiji cha Sakalilo kilichopo kata ya Ilemba, Wilayani Sumbawanga kuhakikisha wanaongeza thamani ya mazao yao ili kuuza kwa bei nzuri nahatimae kusafirisha katika maeneo mbalimbali ya nchi kwani kufanya hivyo kutawapelekea kujitangaza na hatimae kuongeza wigo wa soko.

Ameyasema hayo alipotembelea ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao katika Kijiji cha Sakalilo chenye wakati wapatao 1192, Mradi huo unafadhiliwa na AGRA kupitia mradi wa TIJA na unatekelezwa na sekta binafsi ambao ni shirika la MIIC, ambapo ghala hilo litakuwa na uwezo wa kuhifadhi jumla ya tani 450 na  utagharimu shilingi milioni 155 na kutegemewa kuhudumia wakulima wapatao 500.

“Mfikirie kuyaongezea thamani mazao haya kuna watu wanatokea mikoa ya jirani wanakuja kuchukua mpunga hapa wanakwenda nao kwao halafu wanaongezea thamani na kuandika wa kwao wakati unatoka Sakalilo, hivyo ghala hili lisiwe tu kwaajili ya kuhifadhia mazao kusubiri bei ipande lakini pia mfikirie kuweka mashine kwaajili ya kuyaongezea thamani mazao hayo,” Alisema.

Kwa upande wake Afisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Shabani Bahari alisema kuwa fedha za ujenzi wa ghala hilo zimepatikana kutoka vyanzo mbalimbali na unategemewa kumalizika ndani yam waka mmoja tangu kuanza ujenzi wake.

“Ujenzi huu ulianza tarehe 13.3.2018 na utamalizika tarehe 15.4.2019 na kugharimu shilingi milioni 155 ambapo mpaka sasa milioni 15 ni nguvu ya wananchi, shilingi 700,000/= zimetolewa na Sakalilo AMCOS kwaajili ya kiwanja na Shilingi milioni 80.5 zimetolewa na wafadhili,” Alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Sakalilo AMCOS Osward Sinkala amesema kuwa ghala hilo litakuwa mkombozi kwa wakulima wa kata nzima ya Ilemba na kuongeza kuwa mipango iliyopo ni kukusanya mazao kuanzia mwezi wa 4, na kufafanua kuwa tayari wameshaongea na benki ya NMB ili kuweza kuwawezesha wakulima watakaohifadhi mazao yao kwenye ghala hilo kupata mkopo na pindi bei itakapopanda waweze kuuza na kurudisha mkopo.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa