• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza kutumia bidhaa za viwanda vya ndani kujihakikishia soko.

imewekwa Tar: February 22nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi wa Mkoa wa Rukwa na watanzania kwa ujumla kujenga mazoea ya kutumia bidhaa zinazozalishwa na viwanda vilivyopo kwenye maeneo yao ili kujihakikishia soko la ndani na hatimae kuvuka mipaka ya nchi.

Ameyasema hayo baada ya kutembelea Kiwanda cha Unga Energy Sembe na Kiwanda cha maji Dew Drop vinachomilikiwa na Azizi Mohamed Sudi, Mbasira Fodd Industries na Kiwanda cha maziwa OTC Kizwite kinachomilikiwa na kikundi cha wafugaji vyote vikipatikana katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa vinavyozalisha bidhaa zinazouzwa ndani ya Mkoa, nje ya Mkoa na kuvuka mipaka ya nchi.

Amesema kuwa Kazi ya Serikali kutoa mazingira bora na wezeshi ili wawekezaji wawe na fursa nzuri za kuwekeza na kuongeza kuwa serikali haitakubali kuona viwanda vikifa kwa mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wa serikali na kuwahakikishia wamiliki wa viwanda hao kuwa serikali haiwezi kuendelea kuhamasisha viwanda bila ya kutatua changamoto mbalimbali zinazokumba viwanda vilivyopo.

“Tujivunie viwanda vyetu vya hapa, hasa vile vinavyozalishwa na wazawa wenyewe ambavyo vinatoa ajira kwa wananchi wa Mkoa huu, changamoto zipo kama masuala ya kimazingira, malighafi na umeme, kama serikali tutayachukua ili kuhakikisha wawekezaji wanafanya kazi katika mazingira bora kabisa, kazi ya serikali kuweka mazingira wezeshi ili wenzetu waweke viwanda ili tuweze kufikia uchumi wa kati wa Viwanda kufikia 2025,” Alisema.

Na kushauri kuwa viwanda hivyo havinabudi kujitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ili kuweza kupata masoko ya uhakika.

Kwa upande wake Mmiliki wa Kiwanda cha Unga Energy Sembe na Dew Drop, Aziz Mohamed Sudi amesema kuwa kiwanda cha sembe kimesimama uzalishaji wake tangu Mei, 2017 baada ya kukosa soko la ndani ya nchi na kutegemewa kuanza tena mwaka 2018 baada ya kupata maombi kutoka nchi ya Kongo.

“Wawekezaji katika mikoa ya pembezoni tumekuwa mbali na masoko makubwa, gharama za uzalishaji, umeme na kupeleka bidhaa hizo kwenye masoko makubwa zimekuwa kubwa pamoja na pamoja na utititiri wa kodi, hivyo tunaiomba serikali iruhusu kuuza bidhaa za kiloimo zilizoongezwa thamani na tunakubalina na hatua za kudhibiti chakula kwa kuuza nafaka,” Azizi Alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa