• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza kutumia bidhaa za viwanda vya ndani kujihakikishia soko.

imewekwa Tar: February 22nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi wa Mkoa wa Rukwa na watanzania kwa ujumla kujenga mazoea ya kutumia bidhaa zinazozalishwa na viwanda vilivyopo kwenye maeneo yao ili kujihakikishia soko la ndani na hatimae kuvuka mipaka ya nchi.

Ameyasema hayo baada ya kutembelea Kiwanda cha Unga Energy Sembe na Kiwanda cha maji Dew Drop vinachomilikiwa na Azizi Mohamed Sudi, Mbasira Fodd Industries na Kiwanda cha maziwa OTC Kizwite kinachomilikiwa na kikundi cha wafugaji vyote vikipatikana katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa vinavyozalisha bidhaa zinazouzwa ndani ya Mkoa, nje ya Mkoa na kuvuka mipaka ya nchi.

Amesema kuwa Kazi ya Serikali kutoa mazingira bora na wezeshi ili wawekezaji wawe na fursa nzuri za kuwekeza na kuongeza kuwa serikali haitakubali kuona viwanda vikifa kwa mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wa serikali na kuwahakikishia wamiliki wa viwanda hao kuwa serikali haiwezi kuendelea kuhamasisha viwanda bila ya kutatua changamoto mbalimbali zinazokumba viwanda vilivyopo.

“Tujivunie viwanda vyetu vya hapa, hasa vile vinavyozalishwa na wazawa wenyewe ambavyo vinatoa ajira kwa wananchi wa Mkoa huu, changamoto zipo kama masuala ya kimazingira, malighafi na umeme, kama serikali tutayachukua ili kuhakikisha wawekezaji wanafanya kazi katika mazingira bora kabisa, kazi ya serikali kuweka mazingira wezeshi ili wenzetu waweke viwanda ili tuweze kufikia uchumi wa kati wa Viwanda kufikia 2025,” Alisema.

Na kushauri kuwa viwanda hivyo havinabudi kujitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ili kuweza kupata masoko ya uhakika.

Kwa upande wake Mmiliki wa Kiwanda cha Unga Energy Sembe na Dew Drop, Aziz Mohamed Sudi amesema kuwa kiwanda cha sembe kimesimama uzalishaji wake tangu Mei, 2017 baada ya kukosa soko la ndani ya nchi na kutegemewa kuanza tena mwaka 2018 baada ya kupata maombi kutoka nchi ya Kongo.

“Wawekezaji katika mikoa ya pembezoni tumekuwa mbali na masoko makubwa, gharama za uzalishaji, umeme na kupeleka bidhaa hizo kwenye masoko makubwa zimekuwa kubwa pamoja na pamoja na utititiri wa kodi, hivyo tunaiomba serikali iruhusu kuuza bidhaa za kiloimo zilizoongezwa thamani na tunakubalina na hatua za kudhibiti chakula kwa kuuza nafaka,” Azizi Alisema.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAZAZI WAPATIENI WATOTO ELIMU KUHUSU HEDHI SALAMA

    June 02, 2023
  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa