• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza usafi katika mahindi kujikinga na Kansa.

imewekwa Tar: February 23rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima wote mkoani Rukwa kuhakikisha wanayasafisha mahindi yao kabla ya kuyauza ili kupata soko la uhakika na pia kujiepusha na magonjwa mbalimbali ikiwemo kansa endapo mahindi hayo yatauzwa yakiwa na mchanganyiko wa mahindi yaliyooza na takataka.

Amesema kuwa mahindi yaliyooza yana sumu Kuvu ambayo hutengenezwa yakiwa na upepo na unyevu, sumu ambayo huleta kansa kwenye miili ya binadamu endapo mahindi hayo yatasagwa na athari hiyo haitakuwa kwa watanzania peke yao bali hata walaji waliopo nje ya nchi.

“Muhakikishe kwamba mahindi yale mnayoyachambua hambakishi mahindi yaliyooza na matakataka yale mahindi yaliyooza ni sumu ile inaitwa sumu kuvu inakuja kutengenezwa baadae kukiwa na upepo na unyevu na kusababisha kansa, lakini pia mawe yakiingia kwenye mfumo wa kusaga unga, chakula kikiwa na mawe kitasababisha kidole tumbo, ambapo hadi ufanyiwe upasuaji ndipo upone,” Alisema

Na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo kutasaidia kutangaza bidhaa nzuri zitakazo Mkoa wa Rukwa katika mikoa mbalimbali nchini lakini pia kama usafi huo utazingatiwa utaleta sura nzuri katika soko la kimataifa na hatimae kuitangaza nchi kwa bidhaa zake bora.

Ameyasema hayo alipotembelea kiwanda cha kuzalisha unga cha Mbasira Food Industries kilichopo kata ya Malangali, Wilaya ya Sumbawanga kujionea maendeleo ya kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha tani 36,000 za unga kwa mwaka na kuongea na vibarua wa kiwanda hicho waliokuwa wakitenga mahindi mazima na mabovu kwaajili ya uzalishaji.

Nae Mkurugenzi wa Mbasira food Industries Ltd Mikidadi Kassanda amesema kuwa changamoto kubwa wanayopambana nayo katika kununua mahindi kutoka kwa wakulima ni kupata machanganyiko wa mahindi mabovu na kusababisha kupoteza kilo nne za mahindi mabovu katika kila kilo 100 za mahindi wanayouziwa na wakulima.

“Moja ya changamoto tunazokumbana nazo ni ukosefu wa mafunzo bora kwa wakulima juu ya uzalishaji bora wa mahindi na hatimae kupata mahindi yasiyo na viwango,” Alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa