• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo asisitiza watumishi kutoa elimu ya Corona hadi vijijini baada ya wananchi na vijana wengi kutofuatilia vyombo vya habari.

imewekwa Tar: April 3rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameitaka Kamati ya maafa ya Mkoa kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu kuanzia ngazi ya Kijiji, Mtaa, Kata, Tarafa hadi Mkoa huku akisisitiza mkazo wa kutolewa kwa elimu hiyo uelekezwe kwa vijana ambao wengi wao wanaonekana kutofuatilia taarifa za habari pamoja na elimu mbalimbali zinazotolewa na vyombo vya habari juu ya ugonjwa wa Corona.

Amesema kuwa vijana wa kisasa kuanzia mjini mapaka vijijini wamekuwa wagumu kusikiliza taarifa ya habari kwenye redio wala kuangalia taarifa ya habari kwenye runinga zaidi ya kujiendekeza kusikiliza muziki bila ya kujali na kutaka kujua serikali inasema nini juu ya kujikinga na maradhi hayo ya Corona.

“Akitembea kuna vitu viko masikioni humu anasikiliza muziki tu, nini serikali inasema kuhusu janga hili hajui, lakini mambo haya yanazungumwa sana kwenye redio, yanasemwa sana kwenye televisheni zetu, program ziko nyingi lakini vijana na kundi kubwa wanaonekana hawana muda wa kufuatilia, tuwarudishe hili kundi kubwa, lijenge tabia ya kufuatilia nini kinazungumzwa kwenye redio, kila redio inazungumza, ziko redio za ndani ziko redio zenye sura ya kitaifa,” Alisisitiza.

Aliongeza kuwa hii inaweza kuwa vita ya tatu ya dunia isipokuwa adui hatumuoni hivyo hatuna budi kila mmoja kwa nafasi yake akaendeleza kutoa elimu bila ya kuchoka ili kuweza kupambana na adui huyu ambaye haijulikani lini atashindwa.

Ameyaongea hayo wakati alipofanya kikao na kamati ya maafa ya mkoa iliyowajumuisha waganga wakuu wa wilaya wakiongozwa na mganga mkuu wa mkoa, viongozi wa dini na wataalamu wa ustawi wa jamii pamoja na maendeleo ya jamii wa mkoa na taasisi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na kutoa elimu za afya katika mkoa.

Aidha, Alisisitiza ili kuweza kufanikisha kufikisha elimu kwa wananchi wote wa mkoa huo hakuna budi kuwaelimisha viongozi wa ngazi zote wakiwemo wenyeviti wote wa vijiji na mitaa ili watilie mkazo utekelezaji wa maelekezo ya serikali katika maeneo yao ya kiutawala.

Kuhusu ulinzi wa Mipakani Mh. Wangabo alisema kuwa Mkoa wa Rukwa una vipengo 50 katika ziwa Tanyanyika ambavyo hutumika na wananchi wan hi ya jirani ya Kongo na hivyo kuwataka wananchi kuwa makini na wavuvi wote wanaotoka katika nchi hiyo kuhakikisha wanawarudisha walikotoka na kisha kuripoti kwa vyombo vya usalama na kusisitiza kuwa wananchi wa maeneo hayo wanapaswa kuwa walinzi wa kwanza wa usalama wa nchi yetu.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa