• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo ataka maandalizi ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa kuanza haraka.

imewekwa Tar: December 15th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameiagiza mamlakaya viwanja vya ndege (TAA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kuanza hatua za wali za maandalizi ya uwanja wa ndege wa kimataifa unaotarajiwa kujengwa katika Kijiji cha Kisumba kata ya Matanga, Wilaya ya Sumbawanga.

Amesema kuwa kutokana na ufinyu wa eneo la Kiwanja cha Sumbawanga mjini kinachoendelea na taratibu za kuukamilisha ni vyema mamlaka hiyo ikaanza kutafuta hatimiliki ya uwanja wa Kisumba pamoja na kuweka mipaka inayoonekana katika uwanja huo pamoja na kuendelea kuwazuia wananchi kuvamia na kuendelea na ujenzi.

“Hatua za mwanzo za kupata hati ya hicho kiwanja ziendelee ili eneo hilo limilikiwe kisheria japokuwa lilitengwa tangu miaka hiyo kwaajili ya dhumuni hilo, ili muwazuie wananchi kuvamia maana mji unakua, watu wanongezeka na aerdhi haiongezeki, ili kuwazuia watu hilo lianze haraka,” Alisisitiza.

Eneo la Uwanja wa ndege wa Kisumba lenye ukubwa wa ekari 3411 na umbali wa kilomita 19 toka Sumbawanga mjini, lilitengwa tangu kuanzishwa kwa Mkoa wa Rukwa mwaka 1974 ambalo mpaka sasa hakuna mwananchi aliyevamia na kujenga.

Nae Kaimu Meneja wa uwanja wa ndege wa Sumbawanga Musa Mchola ameeleza kuwa Eneo hilo liliwekewa mipaka kwa alama ya bikon baada ya kutengwa kwa madhumuni ya kuanzishwa kwa uwanja wa ndege ambapo hivi alama hizo zimepotea na baadhi ya watu kuingia na kuanza kulima.

“Eneo hilo lilitengwa mwaka 1974 ila sasa hivi kuna baadhi ya wananchi wa vijiji vya jirani wameingia na kuanza kulima ila baada ya kuongea nao wakafanya Mkutano wa vijiji na kuniandikia barua ya kukiri kuwa wamevamia na kuahidi kuwa hadi mwezi June, 2018 watakuwa wamehama,” alibainisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu amesema kuwa eneo la uwanja wa ndege uliopo katikati yam ji wa Sumbawanga ni dogo la Ekari 74 ukilinganisha na eneo lililopo Kijiji cha kisumba 3411, jambo lililomsukuma Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Rukwa Mhandisi Msuka Mkina kuongeza kuwa mwaka wa Fedha 2018/2019 kutakuwa na upembuzi yakinifu kwaajili ya kujenga uwanja wa kimataifa wa Kisumba na uliopo wa Sumbawanga utatumika kwa matumizi ya “Domestic”.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa