• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atembelea kituo cha Afya na kukuta madudu

imewekwa Tar: November 6th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza mkurugenzi wa halmasshauri ya Wilaya ya Kalambo kuhakikisha anampatia taarifa ya kila wiki juu ya maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya cha Kanyezi, kilichopo kata ya Kanyezi wilayani Kalambo.

Maesema kuwa tangu kuanza kwa miradi ya upanuzi na ujenzi wa vituo vya afya katika halmashauri hiyo kumekuwa na ubabaishaji hasa wa kuchelewa kununua vifaa vya ujenzi pamoja na malipo kwa mafundi ambapo ujenzi huo unatumia mfumo wa “Force Account” kutekeleza kazi hiyo.

“Sasa wewe afisa mipango, Mkurugenzi, kuanzia sasa hivi nataka muwe mnanipa taarifa “on weekly basis” (za kila wiki) kwamba nini kinachoendelea katika ujenzi huu, nisingependa tabia hii ya kusua sua iendelee, muiache mara moja, mnaumiza hawa wajenzi, halafu hamuwezi kuwalipa fidia, ingekuwa hawatimizi wajibu wao ingekuwa kitu kingine, kama ilivyotokea kule Kijiji cha Legeza mwendo fundi akakimbia ni kwasababu ya namna hii ubabaishaji wa malipo, mjipange,” Alisisitiza.

Aliyasema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha afya ambacho kimepandishwa hadhi kutoka kuwa zahanati ya kijiji cha Kanyezi na kukuta zimebaki siku 15 kutakiwa kukabidhi majengo hayo lakini bado wapo katika hatua ya linta.

Kwa upande wake Afisa Mipango wa halmashauri hiyo Bw. Erick Kayombo aliahidi kuwa pamoja na kucheleweshewa kupata fedha lakini halmashauri tayari imeshaagiza vifaa vyote vinavyotakiwa kwaajili ya kumalizia ujenzi.

Kauli hiyo ya Mh. Wangabo ilikuja baada ya mmoja wa mafundi wadogo bw. Hamisi Pesambili kumlalamikia Mkuu wa Mkoa juu ya kucheleweshewa vifaa kwaajili ya kuendelea na ujenzi hali inayowafanya waishi kwa taabu huku wakiwa wameacha familia zao mjini sumbawanga na kwa siku kulipwa shilingi 10,000 fedha ambayo hawaridhiki nayo.

Katika kulirekebisha hilo, Mh. Wangabo alimuagiza mhandisi wa Halmashauri ambaye pia ni msimamizi wa jengo hilo kuhakikisha kuwa wanasimamia malipo ya mafundi wadogo kutoka kwa mafundi wao na sio kuishia kuwalipa mafundi huku hawajui kama vibarua hao wanalipwa kama walivyokubaliana na mafundi wao na kuongeza kuwa kutolipwa vizuri kwa vibarua kunaweza kupelekea majengo kutokuwa na ubora unaotarajiwa.

Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kujenga vituo vitatu vya afya katika halmashauri ya Wilaya ya Kalambo na kutumia zaidi ya shilingi bilioni moja kwaajili ya ujenzi na utanuzi huo huku ikielekeza shilingi bilioni 1.5 kwaajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa