• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atimiza ahadi yake ya kutoa magongo ya kutembelea kwa mlemavu.

imewekwa Tar: April 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametimiza ahadi yake ya kutoa magongo ya kutemebelea kwa Mlemavu Azla Sikazwe Mkazi wa mtaa wa Zimamoto, Kata ya Izia, Wilayani Sumbawanga baada ya mama huyo kumuomba Mkuu wa Mkoa huo msaada wa magongo hayo wakati wa kongamano la watu wenye ulemavu lililofanyika katika Manispaa ya Sumbawanga mwezi wa pili Mwaka huu.

Mh. Wangabo amesema kuwa katika kongamano hilo lilihudhuriwa na walemavu zaidi ya 700 na kusema kuwa bado kuna wengine ambao wanahitaji msaada zaidi na hivyo kuwataka wazazi wote wenye Watoto wenye ulemavu kuhakikisha wanawaibua katika jamii pamoja na kuhakikisha wanawaandikisha shule ili kupata elimu.

“Nitoe wito kwa wananchi wa mkoa wetu wa Rukwa, wawaibue hawa watu wenye ulemavu hasa Watoto ili waweze kupata fursa ya kupata elimu, kwasababu wanayo haki ya kupata elimu ili waweze kulitumikia Taifa, wawaibue kokote walipo ili wawe tayari kwenda shule na sisi kama serikali tupo tayari kuendelea kuwasaidia watu wenye ulemavu, kwa kadiri itakavyowezekana,” Alisema.

Aidha, alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuwa na moyo wa kuwasaidia watu wenye ulemavu ili na wenyewe waweze kujikimu kimaisha kwani kumuwezesha ni mara moja tu ili nae aweze kujiendeleza kimaisha na hivyo wanastahili kusaidiwa.

Kwa upande wake Azla Sikazwe kwanza alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa msaada alioupata, lakini pia aliweza kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa moyo wake wa huruma uliomuwezesha kumsaidia magongo hayo ambayo yatamrahisishia kufanya mizunguko katika shughuli zake mbalimbali za kiujasiliamali.

“Muheshimiwa hapa nimekuja, kweli nashukuru hata sijui niseme nini lakini yote nayaacha mikononi mwa Mungu, na nimekuja mimi ni mjasiliamali lakini, sina chochote hata kuja kwangu nimeomba tu ridhaa kwa mtu ndio akanileta hapa,” Alimalizia.

Katika makabidhiano hayo pia alikuwepo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Mkoa wa Rukwa Ndugu Maria Kalula amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kitendo hicho cha kuweza kumsaidia mama huyo vifaa hivyo ili aweze kufanya shughuli zake na kusisitiza kwa wazazi wote wanaowaficha Watoto walemavu kuacha kitendo hicho na badala yake wajitokeze ili waweze kupatiwa msaada.

“Tendo ambalo amelifanya mkuu wetu wa mkoa nit endo la kihistoria kwakweli, na tunamshukuru sana kwasababu ameona umuhimu wa kuwahudumia walemavu, ni kweli walemavu wako wengi wengine hata bado hawajaanza kutokeza wamefishwa ndani, mi natoa ushauri kwa wale ambao wana Watoto wa aina hiyo, waweze kuwatoa ndani wawatambulishe kwa serikali yetu sikivu, na Mkuu wa Mkoa ameanza naamini ataendeleza hili jambo ili aweze kuwasaidia na wengine,” Alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa