• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atoa mwezi mmoja kuwa na mkakati wa kuzuia uvuvi haramu kuokoa viwanda vya samaki mwambao wa ziwa Tanganyika

imewekwa Tar: January 11th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kalambo pamoja na kamati yake ya Ulinzi na Usalama kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kukaa pamoja na kuandaa mkakati wa kuzui uvuvi haramu unaoendelea katika mwambao wa ziwa Tanganyika ili kuokoa viwanda vilivyopo katika mwambao huo.

Amesema kuwa uvuvi haramu unaoendelea katika mwambao huo unahatarisha maendeleo ya viwanda vya samaki vilivyopo na hatimae kudhoofisha ajira za wananchi waliopo karibu na viwanda hivyo na hatimae kurudisha nyuma juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuibua na kuimarisha viwanda vilivyopo.

“Mwisho wa mwezi huu nataka taarifa ya namna mlivyojipanga kupiga marufuku uvuvi haramu ikiwa ni pamoja na kutoa elimu na kuwakamata wale wanaokaidi na kuendesha uvuvi haramu, uvuvi haramu ukiendelea hiki kiwanda hakitakuwepo, kwasababu ya kuua samaki na watoto wake, achene uvuvi haramu, mnamaliza samaki katika ziwaletu hili,” RC Wangabo Alisisitiza

Ameongeza kuwa samaki ndio rasilimali pekee inayowaajiri pamoja na kuendesha kiwanda na kuwataka wananchi kuungana pamoja kuhakikisha wanatunza rasilimali hiyo, na kupiga marufuku aina zote za uvuvi haramu na kuonya kutosikia kiwanda kimefungwa kutokana na kukosa samaki amabao wamekwisha kwasababu ya uvuvi haramu.

Ameyasema hayo alipotembelea viwanda viwili vya samaki vya Mikebuka Fisheris Tanzania Limited pamoja na Akwa Fisheries Tanzania Limited vilivyopo katika kata ya Kasanga ambapo kiwanda pekee kinachojikongoja ni Mikebuka fisheries huku AkwaFisheries kikiwa kimesimamisha uzalishaji.

Awali alipokuwa akisoma taarifa ya Kiwanda cha Mikebuka Fisheries Tanzania Limited Mtendaji wa Kijiji cha Muzi Gasper Kateka amesema kuwa mbali na ukosefu wa samaki ametaja kuwa changamoto nyingine ni Umeme na barabara jambo linalowafanya kutumia gharama kubwa kendesha kiwanda hicho kwa majenereta na kupakia samaki kwenye boti hadi bandari ya kasanga ili kuweza kuwasafirisha kwenda Sumbawanga kukwepa kipande cha barabara cha Km 1.2 kilichojaa mawe.

“Mikebuka Fisheries in maeneo mawili ya kuchakata samaki ikiwa Sumbawanga yenye uwezo wa kilo 8000 kwa siku na kasanga yenye uwezo wa kilo 15000 kwa siku lakini kutokana na uhaba wa samaki uwezo umeshuka na kuchakata kilo 3000 hadi 4000 kwa siku na kuajiri watu 30 na vibarua 55,” Kateka alieleza.

Kwa upande wake Afisa uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Godfrey Makoki alitoa ufafanuzi wa makubaliano ya matumizi ya ziwa Tanganyika yaliyofanya na nchi nne (Zambia, Burundi, Tanzania na DR Congo) katika kikao kilichofanyika 18/10/2012 Mjini Bujumbura katika kanuni ya nne ya makubaliano hayo imekataza uvuvi wa dagaa mchana katika ziwa Tanganyika.

“jambo linalotupa shida ni uvuvi wa kuvua dagaa mchana, kitaalamu dagaa huwa wanakuja kutaga mchana hivyo wanakuwa wakubwa kwasababu wana mayai na usiku huwaoni, sasa huwa tunawaambia kuwa huo ni uvuvi haramu hapo inakuwa ni tatizo,” Makoki Alibainisha.

Katika Kutatua tatizo la Umeme na Barabara Mh. Wangabo amemuagiza Meneja wa Tanesco Mkoa wa Rukwa kuhakikisha umeme wa REA awamu ya tatu unawafika haraka katika Kijiji hicho kwani kipo kwenye mkakati na kuwaagiza TARURA na TANROAD kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha ndani ya miezi mitatu wanairekebisha barabara ya Km 1.2 ili iweze kupitika.

Mwambao wa Ziwa Tanganyika kwa Mkoa wa Rukwa una Viwanda Vinne vya Samaki, Viwili vipo Kata ya Kipili, Wilaya ya Nkasi na Viwili vipo Kata ya Kasanga, Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa