• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atoa ufumbuzi mgogoro wa ujenzi Kituo cha Afya Samazi

imewekwa Tar: June 21st, 2019

Hatimaye Mkuu wamkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amengilia kati mgogoro wa ujenzi wa kituo cha afya cha Samazi wilayani Kalambo uliodumu kwa zaidi ya miezi miwili baada kutokea kwa mvutano baina ya vijiji vinne huku kila kijiji kikitaka ujenzi ufanyike sehemu yake na hivyo kupelekea uongozi wa halmashauri hiyo kusimamisha harakati za ujenzi huo kwa lengo la kutafuta suluhu.

Kata ya Samazi inapatikana katika mwamabao wa ziwa Tanganyika licha ya hilo kata hiyo imekuwa ikikabiliwa na chanagamoto kubwa ya ukosefu wa kituo cha afya hali ambayo  imekuwa ikiwalazimu wananchi kutembea umbali wa zaidi ya km 20 ili kutafuta huduma za matibabu katika kituo cha afya cha Ngolotwa.

Kwa kuliona hilo serikali ilitoa fedha kiasi cha shilingi million 400 kwa ajili ya ujezi wa kituo cha afya katika maeneo hayo na kutoa maelekezo kwa wananchi kutafuta eneo la ujenzi hali ambayo ilipelekea kila kijiji kutoa mapendekezo yake na huku baadhi yao wakitaka kituo hicho kujengwa juu ya mlima na huku wengine wakiwa na mapendekezo tofauti na kupelekea uongozi wa mkoa huo kuingilia kati suala hilo.

Hata hivyo kabla ya kutoa maamuzi juu ya wapi kituo kijengwe mkuu wa mkoa huo Mh.Joachim Wangabo kwanza akatoa nafasi kwa wananchi kutoa mapenzekezo yao.

Oswald Lwela makazi wa kijiji cha Kisala Alisema kuwa angependa kituo cha afya kujengwa sehemu ya mbele ya kiwanja cha mpira iliyopo juu ya kilima jambo liliungwa mkono na Rosemary Anika mkazi wa Kijiji cha Kipanga Kata ya Samazi.

Baada ya kusilizikiliza maoni ya wananchi Mh. Wangabo alimwagiza mkurugezi mtendaji wa halmashauri hiyo Palela Msongera kuanza ujezi huo mara moja .

“Wote naona mmekubali jipigieni makofi, mimi nimefanya maamuzi, pale ambapo ninyi mmeshindwa kufanya maamuzi mimi nitafanya maamuzi kwa manufaa ya uuma lakini sijafikia huko kwakua mmeshaongea na wataalamu wangu wameshaongea na Kauli zenu wote zinakubaliana, vyote vinasema uwanja wa mpira mabpo mlishaanza kufanya maandalizi,” Alisema.

Kwa upande wake mkurugezi mtendaji wa hamshauri hiyo Palela Msongera amesema wamejipanga kuanza ujenzi huo mapema na kuwa tangu awali walikuwa wakisubiri mapendekezo ya eneo kutoka kwa wananchi kauli iliyoungwa mkono na mkuu wa wilaya hiyo Mh.Julieth Binyura.

Halmashauri ya wilaya ya Kalambo inajumla ya vituo vya afya vinne hivyo kukamilika kwa kituo hicho kutasaidia wananchi husani kutoka mwambao wa ziwa Tanganyika kuondokana na adha ya kutembea umbali mrefu wakati wa kutafuta huduma za matibabu.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa