• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo awatahadharisha vibarua wa miradi mbalimbali juu ya Corona huku akisifu ujenzi wa Vihenge Sumbawanga

imewekwa Tar: April 15th, 2020

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatahadharisha mafundi na vibarua wa mradi wa ujenzi wa vihenge unaojengwa na serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kuwa makini na ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona kwa kufuata maelekezo ya wataalamu afya wawapo katika eneo la kazi na wanaporudi kwenye familia zao.

Amesema kuwa afya ya kila mmoja ni muhimu kutokana na mchango wake katika kujenga nchi na hivyo kuwataka kuwa makini kwa kunawa kila mara hali iliyopelekea kumuagiza meneja wa mradi huo kwa niaba ya Wakala wa majengo nchini (TBA) Mhandisi mkazi Haruna Kalunga kuhakikisha eneo hilo la kazi kunakuwa vifaa vya kutosha vya kunawia maji na sabuni kwa kukanyaga kwaajili ya wafanyakazi na kuondoa ndoo zilizopo ambazo koki zake hazina usalama.

“Afya yako ni ya Msingi sana, na familia yako na sisi sote kwa ujumla wake, kwa maana wewe mtu mmoja ukiugua Corona utaweza kuusambaza kwa watu wengi sana, na wote hapa mnaweza mkafutika ndani ya wiki moja tu, sasa mtakuwa mmeiweka nchi mahali pabaya na mradi wenyewe utasuasua, kwahiyo mjihadhari na ugonjwa huu hatari wa Corona, lakini mchape kazi msiogope kuchapa kazi,” alisema.

Aidha, alitoa pongezi kwa mkandarasi wa mradi huo Unia araj kutoka nchini Poland kwa kusaidiana na mkandarasi mzawa Elerai kutoka Arusha pamoja na meneja wa mradi huo TBA pamoja na mafundi wa mradi huo kwa kufanya kazi ndani ya wakati mbali na hali ya hewa kutokuwa Rafiki kwa ujenzi huo na hivyo kuwataka kuongeza kasi ili kukamilisha ujenzi huo ifikapo tarehe 9.3.2020.

“Ningependa ratiba hiyo izingatiwe, tusirudi nyuma tuongeze kasi kwa kiwango ambacho mradi huu tunataka umalizike mapema, utakuwa na manufaa makubwa sana kwasababu uwezo wa kutunza nafaka zetu kimkoa utaongezeka kutoka tani 30,500 za sasa mpaka kufika tani 55,500 utakuwa ni uwezo mkubwa, kwahiyo hata wakulima wetu watahamasika kulima mahindi zaidi wakijua kwamba NFRA itaweza kuyanunua na kuyahifadhi kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi,” Alisema.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa TBA Mhandisi Mkazi Haruna Kalunga alisema kuwa ujenzi huo utajumuisha majengo 13 ambapo ujenzi wa vihenge 6 vikubwa na vihenge 2 vidogo pamoja na miundombinu yake itachukua asilimia 70 ya mradi huku asilimia 30 ikibebwa na majengo saidizi.

“Kuna Jengo la utawala, kuna jengo la kupikia na kulia chakula, kuna jengo la kutunzia vifaa na dawa, kuna jengo la maabara kwaajili ya upimaji wa hizo sampuli ambazo zitakuwa zinaingia hapa, kuna vihenge 6 vikubwa na vihenge vidogo kwaajili ya usafi vyenye jumla ya tani 20,000 na pia tuna ghala la kuhifadhia mazao lenye uwezo wa kubeba tani 5,000,” alisema.

Kwa mkoa wa Rukwa mradi huo utagharimu Dola za Kimarekani 6,019,399.00 wakati mkandarasi huyo akifanya kazi katika mioa mingine ya Manyara na Katavi ambapo jumla ya gharama yake ni $20,280,906.00 ambapo hadi sasa mkandarasi huyo ameshalipwa $ 10,175,714.22.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa