• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo awatahadharisha wataogushi taarifa ili kupewa vitambulisho vya wajasiliamali

imewekwa Tar: December 19th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukw Mh. Joachim Wangabo amewatahadharisha wafanyabiashara watakaogushi taarifa kwa nia ya kupatiwa vitambulisho vilivyotolewa na Rais Dk.John Pombe Magufuli kwaajili ya wajasiliamali wadogowadogo kote nchini walio na mitaji isiyozidi shilingi milioni nne.

Amesema kuwa jukumu lake ni kuvikabidhi kwa wakuu wake wa wilaya ili nao kuvifikisha kwa wakurugenzi na hatimae kuwafikia walengwa wa vitambulisho hivyo na kuongeza kuwa wajasiliamali waondoe shaka juu ya idadi ya vitambulisho hivyo kwani vikiisha vitaagizwa vingine na hakuna atakaekosa.

“20,000/= kwa kila kitambulisho, lakini kwa mtu yeyote yule ambae atakuwa “amefoji” ambae atapewa kitambulisho bila ya kustahili atanyang’anywa kitambulisho hicho na 20,000/= hazitarudi, kwahiyo nitoe angalizo kwa hawa wajasiliamali wadogo wadogo wazingatie hizo taratibu ambazo zimewekwa,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo katika hafla fupi ya kukabidhi vitambulisho hivyo 25,000, kwa wakuu wa Wilaya tatu za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi zenye halmashauri nne, hivyo kila halmashauri kupatiwa vitambulisho 6,250.

Wakati akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, katibu Tawala wa Mkoa huo Bernard Makali alitahadharisha kuwa vitambulisho hivyo vina alama maalum ambayo haionekani kwa macho na kuonya kuwa wananchi wasijidanganye wala kuthubutu kugushi popote walipo.

Awali akisoma masharti ya kupatiwa kitambulisho hicho Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) mkoa wa Rukwa Fredrick Kanyiriri alisema kuwa miongoni mwa mashari ya mjasiliamali atakayekabidhiwa kitambulisho hicho ni pamoja na mjasiliamali huyo kujaza fomu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kujipambanua kwamba mauzo yake hayafiki shilingi milioni nne kwa mwaka na kulipa shilingi 20,000/= ambayo itaingia katika akaunti kodi za ndani.

Pia alifafanua “Sharti la pili ni lazima mjasiriamali huyo lazima awe hajasajiliwa TRA kwa maana ya hana namba ya utambulisho (TIN) isipokuwa tu kwa wale waliopata namba ya utambulisho huko mwanzoni kwasababau mchakato huu ulianzia TRA wa kuwatambua wajasiliamali hawa lakini lakini baada ya kukwama Mh. Rais aliamua auchukue na kuuweka katika utaratibu mwingine lakini kuna wenye TIN.”

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa