• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo awataka Waganga wa tiba asili na machifu wa Mkoa kuwa mfano katika mapambano dhidi ya Corona

imewekwa Tar: April 7th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza machifu pamoja na waganga wa tiba asili ndani ya mkoa wa Rukwa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona, kwa kuwa na ndoo za maji yanayotitirika na sabuni katika maeneo yao ya kazi ili kuwahamasisha na kuwaelimisha wateja wao wanaowapa huduma kuelewa umuhimu wa kunawa mikono ili kujikinga na ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa haitakuwa na maana kama wamepata elimu halafu hawaitumii hali ambayo hakutakuwa na wa kumlaumu endapo ugonjwa huo utasambaa na kuangamiza watu, alisisitiza kuwa kutowaelimisha wateja wao na kushindwa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ni sawa na kulisaliti taifa, ikiwa serikali inaendelea kutimiza wajibu wake wa kutoa elimu ya ugonjwa huo kwa kutumia njia mbalimbali.

“Kwa upande wa maji mimi kwangu ni agizo, machifu wote muwe na ndoo ya maji tiririka na sabuni, muoneshe mfano, waganga wa tiba za asili, na nyinyi wote kwa umoja wenu mkawe na ndoo za maji tiririka na sabuni na elimu mmeipata vizuri, haitakuwa na maana kama mmepata elimu halafu kule mnakwenda hamuitumii halafu ugonjwa unakuja unatuangamiza, utamlaumu nani na elimu tumekupa, itabidi ujute kwamba wewe ni msaliti, umelisaliti taifa, umemsaliti na mungu pia,” alisema.

Mh. Wangabo ametoa maagizo hayo kwa nafasi yake kuwa kiongozi wa machifu mkoani Rukwa, katika kikao kifupi kilicholenga kutoa elimu ya ugonjwa wa Corona kwa machifu pamoja na viongozi wa waganga wa tiba asili wakiwemo wa Chama cha Waganga/ Wakunga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala Mkoani Rukwa (CHAWATIRU).  

Aidha, Mh. Wangabo aliwataka machifu hao kukemea mila zinazowezesha kusambaa kwa ugonjwa wa Corona kwa haraka, ikiwemo watu zaidi ya mmoja kutumia chombo kimoja kunywa pombe za asili, familia kutumia chombo kimoja kutumbukiza mikono kwaajili ya kunawa, pamoja kutumia chombo kimoja cha kuchotea na kunywea maji katika mtungi.

Halikadhalika aliwataka waganga wa tiba asili kuwa na utatratibu wa kulipwa kwa kutumia huduma za mitandao ya simu ama benki ili kuepuka kushika fedha za wagonjwa ambao hawajulikani ugonjwa wao huku akisisitiza kutotowa dawa zinazopelekea mtu kupiga chafya kwa wingi jambo ambalo sio zuri hasa katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Corona.

Kwa upande wake, kaimu mganga Mkuu wa mkoa wa Rukwa Dkt. Emanuel Mtika aliwatahadharisha kuwa kuwatibu wagonjwa wa Corona ni gharama kubwa sana kiasi ambacho endapo ugonjwa huo utasambaa watu wengi wanaweza kupotea kwa kushindwa kufuata maelekezo ya wataalamu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.

“ Kumtibu mgonjwa mmoja kwa siku ni shilingi milioni 48 na mgonjwa anatakiwa atibiwe kwa siku 15, je sisi huo uwezo tunao, hiki kitu kikitutokea huku sisi tutakwisha na ndio maana namshukuru mheshimiwa mkuu wa mkoa kwa kuona umuhimu wa kuitana ili tuelezane ukweli, hiki kitu kikitokea kwetu tutakwisha, kwahiyo nawaomba sana tutumie zile njia za kawaida za kupambana na hili janga,”Alisema.

Pia aliwataka waganga wa tiba asili pindi hasa wale wanaoishi katika mipaka ya Zambia na Kongo kuhakikisha wanapojiwa na mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa wa corona ni vyema wakamshauri au kumpeleka katika kituo cha afya kwa uchunguzi zaidi, au kuwasilisna na uongozi wa Kijiji kwa hatua zaidi.

Aidha, katika kukazia hilo afisa afya wa mkoa alishauri kuwa endapo mtu hana uwezo wa kununua ndoo ya maji tiririka kutokana na gharama yake anaweza kutumia kibuyu chirizi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa