• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo azigeukia NGOs na CSOs kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda kupambana na umasikini

imewekwa Tar: March 27th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezitaka asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali kuchukulia juhudi za uanziswaji wa viwanda nchini unaofanywa na serikali kama suala mtambuka na ukombozi kwa mwananchi katika kupambana vita dhidi ya Umasikini huku wakizingatia utunzaji wa mazingira na kushirikiana na SIDO.

Amesema kuwa takwimu zinaonesha kwamba takribani hekta 300,000 hadi 400,000 za misitu nchini huharibiwa kwa kuchoma Mkaa. Hivyo njia nyingine na muhimu kuokoa mazingira yetu ni kwa kuanzisha viwanda vya kutengeneza Mkaa kwa kutumia marando ya Mbao, Pumba za Mpunga, Mabua ya mahindi n.k. malighafi ambazo hupatikana kwa wingi Mkoani kwetu.

 “Kwa sababu hiyo ninapenda kutoa wito kwa NGOs na CSOs kushiriki kwenye kampeni hii ya uanzishwaji wa viwanda yenye kaulimbiu ya Mkoa wetu, Viwanda vyetu kwa kuanzisha viwanda. Viwanda tunavyovilenga ni vile vidogo vya thamani ya kuanzia milioni 2 hadi Milioni 10,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Meneja wa SIDO Emanuel Magere amesema kuwa asasi pamoja na mashirika hayo yamekuwa yakitoa elimu mbalimbali kutegemea matatizo ama changamoto za wananchi lakini imefika wakati kutambua kuwa, wananchi hao wanahitaji pia elimu ya ujasiliamali ili kuanzisha viwanda, na kuziomba taasisi za fedha kuweza kutoa mikopo kwa wanaohitaji kuanzisha viwanda.

“Mwamko katika uazishwaji wa viwanda sio mkubwa sana, wengi wamekuwa wakijiwekeza kwenye sekta ya huduma mfano, mashule, migahawa, maduka na huduma mbalimbali ambayo “return” yake inakuwa ya haraka kuliko viwanda na pia changamoto ya masoko ya bidhaa za ndani ya mkoa kutoka kwa bidhaa za nje ya mkoa ama nje ya nchi imekuwa ni changamoto kwa mkoa,” Alimalizia.

Katika kuhimiza ushirikiano Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda amezitaka NGO na CSO hizo kuweza kufika kwenye ofisi za kiserikali ili kuweza kujitambulisha shughuli wanazofanya na kujitokeza kwenye songambele mbalimbali zinazofanywa na halmashauri katika ujenzi wa madarasa ya shule na vituo vya afya ili michango yao ijulikane na sio kusubiri kutafutwa na serikali.

Katika utekelezaji wa viwanda 100, ndani ya kipindi cha miezi minne kuanzia Disemba mwaka 2017 hadi 26, Machi, 2018 Mkoa wa Rukwa umezalisha viwanda vidogo 51 huku lengo la Mkoa ni kuwa na viwanda vingi zaidi ili kuchangia kwa kiasi kikubwa lengo la Kitaifa la kufikia nchi ya Uchumi wa Kati wa Viwanda ifikapo 2025.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa